Na Mboza Lwandiko, Wshington DC
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Imeshiriki Mkutano wa mwaka wa 18 wa Benki ya Dunia unaohusu masuala ya Ardhi na Umaskini, Machi 20 – 24, 2017 – Washington DC – Marekani.
Mkutano huo unaobeba ujumbe; “Utawala bora wa Ardhi”, umejumuisha zaidi ya wajumbe 1,200 kutoka nchi wanachama, zilizohusisha Serikali, taaluma, jamii na Sekta binafsi mbalimbali.
Pamoja na mambo mengine; Mkutano huo umejikita zaidi katika Maboresho mbalimbali yanayoendelea kufanyika katika Sekta ya Ardhi Duniani, ikiwa ni pamoja na kuzingatia nafasi ya takwimu na shuhuda zinazoashiria maboresho katika Sera za Ardhi, na kuainisha Mikakati ya Maendeleo katika kuboresha zaidi Sekta ya Ardhi.
Aidha, Mada ambayo imewasilishwa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imewasilishwa na Katibu Mkuu wa Wizara; Dkt. Yamungu Kayandabila, ambayo ilibeba ujumbe -  “Ardhi; Ufunguo wa Utawala Bora na Maendeleo ya Uchumi kwa Tanzania”. Alieleza kuwa utawala wa Ardhi Tanzania unazingatia; Sheria, Uwazi, Uwajibikaji na Ushirikishwaji wa Wananchi. Pamoja na mengine Dkt. Kayandabila alieleza jitihada mbalimbali ambazo zimekuwa zikifanyika kuboresha sekta ya ardhi nchini na juhudi ambazo zinaendelea kuboresha utawala bora wa Ardhi nchini. 
 Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Dkt. Yamungu Kayandabila akiwasilisha mada: “Ardhi; Ufunguo wa Utawala Bora na Maendeleo ya Uchumi kwa Tanzania”. Katika Mkutano wa 18 wa Benki ya Dunia wa masuala ya Ardhi na Umaskini; Washington DC, Marekani.
 Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Dkt. Yamungu Kayandabila, akiwa ameambatana na Mkurugenzi msaidizi wa Idara ya Mipango Miji na Vijiji; Immaculate Senje, Kaimu Msajili wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya ; Amina Rashidi, wakijadili jambo na wajumbe wenzao wa Mkutano wa 18 wa Benki ya Dunia wa masuala ya  Ardhi na Umaskini; Washington DC, Marekani 
 Wajumbe kutoka Tanzania katika picha ya pamoja na ujumbe kutoka Finland kwenye mkutano wa 18 wa Benki ya Dunia kuhusu masuala ya Ardhi na Umaskini uliofanyika mjini Washington DC, Marekani
 Wajumbe kutoka Tanzania wakifanya mazungumzo ya pamoja na mtaalamu mwelekezi wa Benki ya Dunia kutoka nchini Uganda; Bwn. Moses Kibirige (aliyevaa miwani) kwenye mkutano wa 18 wa Benki ya Dunia kuhusu masuala ya Ardhi na Umaskini uliofanyika mjini Washington DC, Marekani
Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Dkt. Yamungu Kayandabila, akiwa na wajumbe wengine kutoka nchi mbalimbali katika vikao vinavyoendelea katika Mkutano wa 18 wa Benki ya Dunia kuhusu masuala ya Ardhi na Umaskini uliofanyika mjini Washington DC, Marekani. Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...