Na
Mary Gwera, Mahakama
KAIMU Jaji Mkuu wa
Tanzania, Prof. Ibrahim Juma ameutaka
Uongozi mpya wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) kuusoma na kuuelewa Mpango
Mkakati wa miaka mitano wa Mahakama ya Tanzania ili umoja huo uweze kuchangia katika
utekelezaji wake.
Prof. Juma aliyasema
hayo mapema leo, Ofisini kwake, Mahakama ya Rufani jijini Dar es Salaam
alipotembelewa na Uongozi wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) ukiongozwa na
Rais wa Chama hicho, Mhe. Tundu Lissu.
Alisema kuwa ni vyema
kuusoma Mpango Mkakati huo ili kufahamu ni wapi Mahakama inatoka na wapi
inapotaka kuelekea hususani katika suala zima la maboresho ya huduma ya utoaji
haki nchini.
Mpango Mkakati wa
Mahakama ya Tanzania (2015/2016-2019/2010) umegawanyika katika nguzo kuu tatu
ambazo ni Utawala bora, uwajibikaji na usimamizi wa rasilimali, Upatikanaji na utoaji haki kwa wakati na
Kurejesha imani ya jamii na ushirikishwaji wa wadau, umejikitika katika kuboresha huduma za utoaji
haki kwa ujumla.
Kwa upande wake, Rais
wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS), amemueleza Mhe. Kaimu Jaji Mkuu kuwa
lengo la ujio wao ni kujitambulisha kwake na pia kumpa pongezi Mhe. Kaimu Jaji
Mkuu kwa kuteuliwa kushika wadhifa huo.
Mbali na utambulisho,
Mhe. Tundu Lissu alipata wasaa wa kueleza baadhi ya changamoto zinazowakabili
Mawakili nchini ikiwa ni pamoja na baadhi ya Mahakama kutokuwa na Ofisi kwa
ajili ya Mawakili, taratibu za usajili wa Mawakili n.k
Akijibu kuhusu hoja ya
Rais wa TLS; Msajili; Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Ilvin Mugeta alisema kuwa
Mahakama Kuu inaendelea kufanyia kazi changamoto zote zinazowakabili Mawakili
na vilevile kuona uwezekano wa taratibu za malipo kufanyika kielektroniki.
Kaimu
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Juma (aliyeketi mbele) akiwa pamoja
na baadhi ya Viongozi wapya wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS)
waliomtembelea kwa lengo la kujitambulisha kwake kama Uongozi mpya na pia
kumpongeza Mhe. Kaimu Jaji Mkuu kwa uteuzi wake, aliyeketi kushoto kwa Mhe.
Kaimu Jaji Mkuu ni Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand
Wambali na aliyeketi kushoto kwa Kaimu Jaji Mkuu ni Rais wa Chama cha Mawakili
Tanganyika (TLS), Mhe. Tundu Lissu.
Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Juma
akiongea jambo na Uongozi wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS)
walipomtembelea Ofisini kwake kwa lengo la kujitambulisha.
Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika, Mhe. Tundu
Lissu akiongea jambo, Ofisini kwa Mhe. Kaimu Jaji Mkuu walipofika kwa ajili ya
utambulisho wa Uongozi mpya wa Chama hicho.
Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania (wa sita kushoto) akiwa
katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi wa Chama cha Mawakili Tanganyika
(TLS) walipomtembelea Ofisini kwake kwa lengo la kujitambulisha, wa tano
kushoto ni Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, wa kwanza kushoto ni
Msajili, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ilvin Mugeta na wa tano kulia ni Rais
wa Chama hicho, Mhe. Tundu Lissu.(Picha na Mary Gwera)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...