Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania UWT, Amina Makilagi
akizungumza na waandishi wa habari, leo, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya
CCM, Lumumba, Dar es Salaam.
Bi
Makilagi alizungumza mambo mbalimbali ikiwemo na kutoa pongezi nyingi
kwa Kamati Kuu ya Halmashauri kuu ya Taifa ya CCM ikiongozwa na
Mwenyekiti wake,Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa uamuzi wake wa kuteua
wagombea wa Ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki kwa uwiano ulio sawa
baina ya Wanaume na Wanawake.
Bi
Makilaki amesema kuwa UWT inawahamasisha Wanachama wake wana CCM wenye
sifa kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika
uchaguzi wa ndani wa chama na Jumuiya zake ambapo kwa UWT Uchaguzi wa
ngazi ya Tawi utaanza April mosi mpaka 10/2017.
Taarifa zaidi hii hapa chini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...