Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania UWT, Amina Makilagi akizungumza na waandishi wa habari, leo, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam.

Bi Makilagi alizungumza mambo mbalimbali ikiwemo na kutoa pongezi nyingi kwa Kamati Kuu ya Halmashauri kuu ya Taifa ya CCM ikiongozwa na Mwenyekiti wake,Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa uamuzi wake wa kuteua wagombea wa Ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki kwa uwiano ulio sawa baina ya Wanaume na Wanawake.

Bi Makilaki amesema kuwa UWT inawahamasisha Wanachama wake wana CCM wenye sifa kujitokeza kwa wingi  kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa ndani wa chama na Jumuiya zake ambapo kwa UWT Uchaguzi wa ngazi ya Tawi utaanza April mosi mpaka 10/2017.

Taarifa zaidi hii hapa chini.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...