Waziri wa Wizara ya Mambo
ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Lameck Nchemba
akiwa pamoja na Watendaji Wakuu wa
Wizara yake wakati wa Kikao cha Mapitio ya Bajeti ya Taasisi ziliko katika Wizara hiyo.
Baadhi ya Watendaji Wakuu
wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakipitia
bajeti za taasisi zao, ikiwa ni sehemu
ya maandalizi muhimu kabla ya kuanza kwa Vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, linalotarajiwa kuanza mapema tarehe nne mwezi Aprili
mwaka huu, wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi
Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa [NIDA] Massawe, akifuatiwa na Kamishna
Jenerali wa Uhamiaji Dr. Anna Peter
Makakala, watatu kushoto ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias
Andengenye na wanne ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Dr. Juma Malewa. Kikao
hicho kimefanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.
IMEANDALIWA
NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI
WIZARA
YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...