Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt. Asha - Rose Migiro leo aliandaa hafla fupi katika makazi ya Balozi kumpongeza kijana mtanzania Alphonse Simbu alieshika nafasi ya tano katika mbio za "London Marathon" zilizofanyika tarehe 23 Aprili 2017 jijini London.
Katika salamu zake, Balozi Migiro alimpongeza Bw. Simbu kwa heshima aliyoipa Tanzania jijini London na Duniani kupitia mbio za London. alimsihi atumie matokeo hayo kama hamasa ya kufanya bidii zaidi kwa ajili ya mashindano ya mbio ndefu anayotarajiwa kushiriki baadae mwakani.
Simbu alimshukuru Balozi Migiro Kwa ushirikiano mkubwa wa kibalozi alioupata akiwa jijini London.Alimkabidhi Balozi Fulana ya kumbukumbu ya ushiriki wake kwenye mbio hizo.
Pichani Balozi Asha Rose Migiro akipokea Fulana hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...