Ndugu zangu, vijana wenzangu wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) na vijana wote wenye mapenzi mema na chama chetu na Watanzania wote kwa ujumla.

Nitangulie kwa kuwashukuru kamati ya utekelezaji ya UVCCM TAIFA kwa kuonyesha mapenzi makubwa na imani kubwa kwangu kwa kukubali kuniteua ku-kaimu nafasi ya Katibu wa UHamasa na Chipukizi. 

Imani yenu kwangu inabaki kuwa deni na chachu ya kujitoa kwa nguvu zote, kwa akili zote kuitumikia vizuri nafasi hii. Mwenyezi Mungu anisaidie.

Pili, kama ilivyo alama ya kwenye nembo ya jumuia yetu, ile alama ya mwenge wa uhuru. Mwenge wa Uhuru unaashiria nuru na mwanga. Mwenge huu unamulika nchini na nje ya mipaka ili kuleta matumaini pale ambapo kuna kukata tamaa, upendo pale kwenye chuki na heshima pale penye dharau- hii nimenukuu. 

Hivyo sifa kuu ya mwenge wetu wa uhuru kwenye nembo ya jumuiya yetu ya vijana ni kutoa mwanga, na sifa kuu ya mwanga ni kuweza kutokomeza giza na kutoa tumaini. Hivyo sisi kama vijana tunategemewa kuwa tumaini. Sisi kama vijana tunategemewa kuonyesha si tu njia bali kuwa tumaini kwamba taifa lilioasisiwa na waasisi wa nchi hii "our founding fathers" lipo katika mikono salama. 

Na hatuishii hapo bali jukumu la kuleta tumaini hili liko kwenye sehemu sahihi kupitia jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama chetu Cha Mapinduzi. Sehemu pekee ambapo viongozi wa sasa na baadae hupikwa vilivyo kuweza kuitumikia nchi yetu kwa weledi na uadilifu uliotukuka. Hivyo basi ni lazima kutengeneza taswira itakayowapa hamu vijana wa Tanzania kutamani kuwa sehemu ya UVCCM. Ni lazima tuwe wabunifu na kuvutia vijana wengi zaidi ili kupanua wigo wetu pia. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...