Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo amewaongoza wakazi wa manispaa ya Singida katika kuadhimisha miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa kufanya usafi katika sehemu mbalimbali za mji wa Singida. 

Akizungumza baada ya kumalizika kwa zoezi la usafi, Tarimo amesema Watanzania wakiwemo wa wilaya ya Singida wanapaswa kuuenzi Muungano huu kwa kushiriki kikamilifu maadhimisho yake. 

Amesema bila Muungano huu ulioasisiwa na viongozi wetu hayati mwalimu Nyerere na mzee Abeid Karume, Tanzania ya leo isingekuwepo. 

“Maadhimisho haya sasa yameboreshwa kwa maana yanaweza kufanyika kwa kufanya usafi kama tulivyofanya sisi leo au kwa mazoezi ya mwili. Niwasihi tu Watanzania wenzangu kuyathamini maadhimisho haya na kushiriki bila kukosa kila mwaka”, amesema. 

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida Bravo Lyampembile amesema wananchi wa manispaa hiyo wamejitokeza kwa wingi na kushiriki vema kuadhimisha siku kuu ya Mungano. 

“Ofisi yangu nayo imeshiriki watumishi wote ambao kwa siku ya leo afya zao ziko vizuri, wamejitokeza na kufanya usafi kama njia ya kuadhimisha siku kuu ya Muungano”, amesema Bravo.
Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo (mwenye kofia nyeupe) akiongoza wakazi wa Manispaa ya Singida kuadhimisha miaka 53 ya Muungano kwa kufanya usafi sehemu mbalimbali za mji wa Singida jana. Mwenye gloves nyekundu ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida Bravo Kizito Lyampembile. 
Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo (mwenye kofia nyeupe) akihimiza Watanzania kujenga utamaduni wa kushiriki maadhimisho ya Muungano wa Tanzania ili kuuenzi. Mwenye gloves nyekundu ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida Bravo Kizito Lyampembile. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...