Nteghenjwa Hosseah, Arusha
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo amekabidhi hundi ya
Tsh Bil 1 kwa vikundi vya wanawake na Vijana ikiwa ni mchango wa asilimi kumi
(10%) ya mapato ya Halmashauri Jiji la Arusha.
Akikabidhi hundi hiyo kwa Vikundi 269 ambavyo kati ya hivyo 162 ni Vikundi vya
wanawake na 107 ni vijana amewataka kutumia fedha hizo kwa shughuli
zilizokusudiwa ili ziweze kuwatoa katika lindi la umasikini.
“Mikopo hii inatolewa ili kuendeleza shughuli za kijasiriamali ambazo ndizo
zilizopelekea mkidhi vigezo vya kupata Fedha; Nimatumaini yangu fedha hizi
zitawawezesha kuongeza mitaji yenu na kuwapa ari ya kujituma zaidi huku
mkizingatia nidhamu ya pesa ili muweze kuzirejesha kwa wakati na makundi
mengine waweze kupata fedha hizo”Alisema Rc Gambo.
Mikopo hiyo inayotolewa kwa mujibu wa Sheria na miongozo inayoelekeza
asilimia kumi ya Mapato ya ndani ya Halmashauri kutolewe kama Mikopo ya riba
nafuu kwa vikundi vya wananwake na vijana na kwa jiji la Arusha kiasi
kinachotakiwa kutolewa ni Bil 1.2 kwa Mwaka huu wa Fedha hivyo kiasi
kilichotolewa ni kwa kipindi cha robo tatu kuanzia Julai 2016 – March 2017.
Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa Mhe. Gambo amekabidhi vitambulisho 3850
kwa Wazee wa kuanzia miaka 60 ambao ni wakazi wa Jiji la Arusha
vitakavyowasaidia kutambulika katika Vituo vvya Afya na kupatiwa huduma za
Afya bure.
Kukabidhi kwa Vitambulisho hivyo kunafanya jumla ya Idadi ya vitambulishbo
vilivyotolewa na Jiji kwa wazee kufikia 5966 na bado zoezi hili linaendelea
kuwabaini wazee wote na kuwatengenezea vitambulisho.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo(katikati)
akiwakabidhi wawakilishi wa Vikundi vya Wanawake na Vijana mfano wa
hundi ya Tsh Bil 1 wakati wa Ziara yake Jijini hapa .kulia kwake ni Mkuu
wa Wilaya Mhe. Gabriel Daqaro na Kushoto ni Mkurugenzi wa Jiji
Athumani Kihamia.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo (katikati kulia)
akimkabidhi Mzee Zahran Mtweike (Mbele kulia) Kitambulisho cha
Wazee.
Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Athumani Kihamia(kulia) akiteta Jambo na
Naibu Meya wa Jiji Mhe. Viola Likindikoki wakati wa Ziara ya Mkuu wa
Mkoa Jijini hapa.
Diwani pekee wa Cccm katika Jiji la Arusha Mhe. Abdulrasul Tojo (mbele)
akifuatilia nkikao cha Mkuu wa Mkoa wakati wa siku ya kwanza ya ziara
yake Jijini hapa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...