Na Karama Kenyunko, blogu ya jamio.

Rais wa Jamuhuri y Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli anatarajiwa Kuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya Uhuru wa Habari Mei mwaka huu.

Maadhimisho hayo ya mwaka huu, yatafanyikia jijini Mwanza kwa Siku mbili mfululizo kuanzia Mei 2 na 3 mwaka huu yakiwa na maudhui yanayosema fikra yakinifu kwa wakati muhimu'.

Akizungumzia madhimisho hayo, Mwenyekiti wa Misa Tanzania Salome Kitomary amesema lengo la siku hiyo ni kuwakutanisha wadau wa Habari kuweka msukomo wa mataifa kutunga sheria za vyombo vya habari ambazo zinahakikisha Uhuru wa habari katika nchi husika.

 Amesema lengo lingine ni kufikia makubaliano ya kitaifa juu ya kuanzisha utaratibu wa usalama na ulinzi wa wanahabari na wafanyakazi wa vyombo vya habari kwenye mtandao na nje ya mtandao.
Aidha Aliongeza kuwa lengo lingine ni kutetea Sera na mfumo wa mageuzi ya kisheria kwa ajili ya vyombo vya Habari na maendeleo endelevu.

Kwa upande wake makamu wa rais kutoka umoja wa clabu za waandishi Tanzania, UTPC, Janne Mihanji amewataka waandishi wawe ndio wapangaji wa ajenda za taifa badala ya kutumiwa na wanasiasa.
Aidha amewaasa waandishi wakiwa katika maeneo yao kazi, kuchukua tahadhari wakiangalia usalama wao zaidi kwani hakuna habari bora kuliko uhai wa mtu mwenyewe. Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika-Tanzania, Salome Kitomari akizungumza kwenye mkutano wa wanahabari kutambulisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari 2017 uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika-Tanzania, Salome Kitomari akizungumza kwenye mkutano wa wanahabari kutambulisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari 2017 uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Makamu Rais wa UTPC, Bi. Jane Mihanji na Mwenyekiti wa Klabu ya Waandushi Dar es Salaam akizungumza katika mkutano wa wanahabari kutambulisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari 2017 uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Baadhi ya wanahabari na wageni waalikwa wakiwa katika mkutano na Kamati ya maandalizi ya WPFD-2017 kutambulisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari 2017 uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...