Jumuiya ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii nchini kupitia (TSSA) inayoundwa na Mifuko ya NSSF, PPF, LAPF, PSPF, GEPF, NHIF, WCF pamoja na ZSSF imefanya ziara ya kutembelea
kiwanda cha nyama kilichopo mjini Shinyanga ambacho hakikuwahi
kufanya uzalishaji tangu kibinafisishwe, lengo la Ziara hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya kuona hali halisi ya kiwanda hicho ambacho kwa
sasa kipo chini ya mikono ya Serikali, Mifuko hiyo kwa pamoja kupitia
umoja wao wa TSSA wamedhamiria kuwekeza kwa pamoja katika sekta
ya ngozi, nyama na nguo katika kiwanga hivyo. wanaonekana mbele ni Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Adam Mayingu (wa pili kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa GEPF, Daud Msangi (wa pili kulia).
Jumuiya ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii nchini kupitia (TSSA) inayoundwa na Mifuko ya NSSF, PPF, LAPF, PSPF, GEPF, NHIF, WCF pamoja na ZSSF wakipatiwa maelezo wakati
walipotembelea kiwanda cha nyama kilichopo mjini Shinyanga, ambacho
hakikuwahi kufanya uzalishaji tangu kibinafisishwe.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa GEPF, Daud Msangi akisaini kitabu wakati walipotembelea
kiwanda cha nyama kilichopo mjini Shinyanga, ambacho hakikuwahi kufanya
uzalishaji tangu kibinafisishwe. Kulia ni Mratibu wa ziara hiyo kutoka TSSA, Meshack Bandawe.
Wakuu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii nchini kupitia Jumuiya yake ya TSSA
(Tanzania Social Security Association) wakiendelea na ziara yao katika
kiwanda cha nyama kilichopo mjini Shinyanga.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...