Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mh. William Lukuvi amefanya ukaguzi wa mfumo wa kodi ya ardhi katika manispaa ya Musoma Mjini mkoa wa Mara ambapo amebaini wananchi 231 wanadaiwa Kodi ya Pango la Ardhi kiasi cha shilingi milioni 271.
Mhe Lukuvi amemtaka Afisa Ardhi wa manispaa ya Musoma bwana Joseph Kamonga kuwasilisha majina ya wadaiwa hao katika Mahakama ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kupiga mnada majengo na mali zao kawa wakikaidi kulipa kodi hiyo.
“Nimeagiza kesi za madai ya kodi zitolewe hukumu ndani ya siku moja tu ili wadaiwa waweze kuchukuliwa hatua ya kuuzwa kwa mali zao haraka” Mhe Lukuvi aliyasema hayo wakati alipo fanya ziara ya kukagua mfumo wa kodi wa manispaa ya Musoma mjini ili kuhakikisha wamiliki wote wa ardhi nchini wanalipa kodi kwa hiari kabla ya hatua za kisheria hazijafuata dhidi yao.
Aidha, Waziri Lukuvi amefanya uzinduzi wa mpango kabambe (Master Plan) wa Manispaa ya Musoma na kuwapongeza viongozi na watendaji wa manispaa ya Musoma kwa kuwa manispaa ya kwanza nchini kuweza kuzindua mpango kabambe wa mji wao. Pia aliwapongeza kwa uzalendo wao wa kutumia kampuni za ndani katika utekelezaji wa mpango huo.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi akikagua mfumo wa kodi wa Manispaa ya Musoma Mkoani Mara. Kushoto kwake Afirsa Ardhi wa Manispaa hiyo Ndugu Joseph Kamonga akimuonesha mfumo wa kodi unavyofanya kazi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi akikambidhi Mpango Kabambe wa Manispaa ya Musoma Meya wa Manispaa ya hiyo Mh. Patrick Gumbo.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi akizindua Mpango Kabambe (Master Plan) Manispaa ya Musoma Mkoani Mara.
  Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi akiongea na viongozi na wananchi wa Manispaa ya Musoma katika uzinduzi wa Mpango Kabambe wa Manispaa hiyo.
Baadhi ya Wananchi na Watendaji wa Manispaa ya Musoma wakimsikiliza Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi katika uzinduzi wa Mpango Kabambe wa Manispaa hiyo mkoani mara. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...