WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu
amesisitiza kuwa wanafunzi wa kike wanaopata mimba wakiwa mashuleni waendelee
na masomo yao ili kufikia malengo walioyanayo nchini.
Ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa maswala ya kijinsia
ulioandiliwa na Chuo Cha Ualimu (DUCE) alipomuwakilisha Makamu wa Rais wa
Jamhuri8 ya Muungano waq Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo jijini Dar es
salaam.
“Tunapokataza watoto wa kike wasiendelee na masomo pindi wanapopata ujauzito
wakiwa mashuleni tunawaadhibu watoto wa masikini washindwe kutimiza malengo
yao kwa wakati waliotarajia”alisema Waziri Ummy.
Aidha Waziri Ummy amesema kuwa anaunga mkono uamuzi wa Rais wa Tanzania Dkt.
Jonh Pombe Magufuli kwa kutoa elimu bure nchini kwani kunaongeza idadi ya watoto
wa kike kuwepo mashuleni tofauti na kipindi cha nyuma.
Mbali na hayo Waziri Ummy ametoa wito kwa wazazi kuwahamasisha watoto wao wa
kike kupenda masomo ya sayansi ili kukuza rasilimali watu katika kujenga uchumi
unaotokana na viwanda nchini.
Kwa upande wa Mkuu wa Chuo cha DUCE Prof. William Anangisye amesema kuwa
lengo la mkutano huo ni kuleta chachu ya kuwatia moyo wanafunzi wa kike kupenda
masomo ya sayansi ili kupata wanasayansi wanawake nchini.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na watoto Mh. Ummy Mwalimu akimuwakilisha
Makamu wa Raisi Bi Samia Suluhu Hassan katika ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa Masuala ya
Usawa wakijinsia ulioandiliwa na Chuo Cha Ualimu (DUCE) jijini Dar Es salaam.
Prof Rwekaza Mukandala Makamu Mkuu wa Chuo kikuu cha Dar Es Salaam akihutubia wadau na
wanafunzi waliojitokeza katika mkutano wa kwanza wa masuala ya Jinsia na Usawa yaliyofanyika
katika chuo kikuu cha Uwalimu DUCE jijini Dar Es Salaam.
Mkuu wa Chuo cha DUCE Prof. William Anangisye akihutubia jopo la Wadau na
wanafunzi katika mkutano wa masuala ya Usawa na huku akisisitiza wazazi na walezi
kuwatia moyo wanafunzi wa kike kupenda masomo ya sayansi ili kupata wanasayansi
wanawake nchini.
Wadau wa Masuala ya Usawa wa kijinsia wakifuatilia kwa ukaribu ujumbe uliokuwa
ukitolewa na Mh.Ummy Mwalimu Waziri wa Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee
na watoto aliyekuwa akimuwakilisha Makamu wa Raisi Bi Samia Suluhu Hassan katika viunga vya
Chuo cha Uwalimu DUCE jijini Dar Es Salaam.
Picha ya pamoja ya wadau wa masuala ya Usawa wakijinsia katika mkutano wa kwanza wa
masuala ya Usawa wakijinsia uliowakutanisha kujadili na kuhamasisha juu ya kumlinda
mtoto wa kike ili apate Elimu sawa kama ile apatayo mtoto wakiume katika jamii yetu.
Asanteni kwa coverage nzuri.
ReplyDelete