BAADA ya kuonekana hali ya kuashiria kupoteza mvuto kwenye tasnia ya filamu hapa Bongo, hatimaye Candyimax imekuja kwa kasi ya kurudisha hadhi ya filamu za hapa nchini na Afrika Mashariki kwa ujumla.

Kupitia ‘Candyimax online streaming Tv’ imetoa fursa kwa kiwanda cha filamu hapa nchini na wadau wote kupeleka miongozo ya filamu (script)  mbalimbali ambazo zitakuwa kwenye ubunifu wa hali ya juu na kuhakikisha wanafanya kazi nzuri zenye viwango ambazo zitaipeleka tasnia hiyo kimataifa.

Katika kutilia mkazo suala hilo Candyimax Tv imejipanga kugharamia muongozo wa filamu (script) ambazo zimepitishwa na uongozi wa Tv hiyo yenye mpango na kusudio kubwa la kuinasua tasnia hiyo ambayo haifanyi vizuri sokoni kwa sasa.

Pia mfumo huo mpya wa kuangalia Tv hiyo online utasaidia filamu hizo kuonekana duniani kote,kwa wahusika wa tasnia hiyo wanatakiwa kuwasilisha kazi zao (script) ofisi zao zilizopo Masaki,barabara ya Umoja wa Mataifa,na kwa mawasiliano zaidi wapigie kwa namba +255765802457.
Baadhi ya wadau wa filamu wakiwa kwenye harakati za maandalizi ya movie mpya

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...