Roger Moore, muigizaji
marufu wa sinema aba za ujasusi za James Bond kati ya mwaka 1973 na 1985,
amefaruiki dunia kwa ugonjwa wa saratani, kwa mujibu wa familia yake. Amefariki
akiwa na umri wa miaka 89.
"Tunajua kwamba mapenzi yetu kwako na kuhusudiwa vitakuzwa mara
nyingi ulimwenguni kote na watu waliomfahamu kutokana na filamu zake, maonesho
katika TV na ukereketwa wake kwa kuifanyia kazi UNICEF ambayo aliamini ni
fanaka kubwa katika maisha yake", watoto wake Deborah, Geoffrey na Christian,
wamesema katika taarifa iliyowekwa kwenye akaunti yake rasmi ya Twitter siku ya
Jumanne.
Familia hiyo itafanya mazishi yake ya kifamilia huko Monaco, kama alivyohusia
yeye mwenyewe, taarifa hiyo inaeleza.
Marehemu Moore alijulikana zaidi kama mtu aliyemrithi muigizaji
Sean Connery katika mlolongo wa sinema za James Bond.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...