Mfuko wa
Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), umeendesha semina ya siku moja kwa waajiri nchini, ili kutoa elimu juu ya shughuli za Mfuko na wajibu wa waajiri
kwa wafanyakazi wao katika kujisajili na kuwalipa michango kwa niaba ya
waajiriwa wao.
Akizungumza
katika semina hiyo mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko Dkt. Francis Michael .
Amesema
kuanzishwa kwa mfuko huo kumekuja wakati muafaka ambapo Tanzania inaelekea
katika uchumi wa viwanda hivyo kupelekea ongezeko la wafanyakazi ambapo chombo
hicho ndio mkombozi wa majanga yatokanayo na kazi.
“Ni muda
muafaka kwa waajiri kutambua wajibu wenu katika Mfuko huu na pia kutambua
madhara ya kutotekeleza wajibu wenu” Alisema Dkt. Michael.
Katika hotuba
yake, Dkt. Michael alieleza umuhimu wa waajiri kuwalipia michango wafanyakazi
wake kama sheria inavyotaka, ili kuwawekea akiba pindi wapatapo na majanga
wakiwa kazini.
Mfuko wa
Fidia kwa wafanyakazi ni Taasisi ya Serikali chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na
umeundwa kwa mujibu wa kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa wafanyakazi Sura
ya 263 iliyorejewa Desemba, Mwaka 2015.
Dkt. Michael
amesema, Mfuko umeamua kuandaa semina hiyo ili kutoa elimu zaidi kwa
waajiri kwa kutambua kuwa waajiri ndio
wadau wakuu wa Mfuko huo na semina hiyo itawasaidia kujua kazi za Mfuko lakini
pia wajibu wa waajiri kwa wafanyakazi katika kutoa michango ya kila mwezi.
Mjumbe wa Bodi wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Dkt. Francis Michael akifungua Semina ya uelimishaji kwa Waajiri kuhusu haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi jijini Morogoro leo, kulia ni Mwanasheria Mwandamizi Bi. Irine Mungu.
Mwanasheria Mwandamizi Bi. Irine Mungu kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) akitoa mada kwa waajiri kuhusu haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi jijini Morogoro leo.
Afisa Uhusuano Mwandamizi kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) akitoa mada katika semina ya uelimishaji kwa waajiri kuhusu haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi mkoani morogoro leo.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...