Na Nteghenjwa Hosseah - Arusha 
Shule ya msingi Lucky Vicent yaibuka na mshindi wa Jumla Kitaaluma kwa kushika nafasi ya kwanza Kimkoa katika maadimisho ya Juma la Elimu yaliyoadhimishwa katika viwanja vya Arusha School jijini hapa. Shule hiyo iliyopata na msiba wa wanafunzi 32, walimu 2 pamoja na dereva kutokana na ajali hivi karibuni imefanya vizur katika mitihani ya darasa la saba iliyofanyika mwaka 2016 katika ngazi ya Mkoa na Wilaya hivyo kujinyakulia Kombe pamoja na Cheti. 
Akipoka zawadi hizo za Ushindi Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Bw. Innocent Mushi alisema wanafarijika kupata zawadi hizo ingawa bado simanzi na majonzi yametanda shuleni kwa wanafunzi pamoja na uongozi wa shule hiyo. 
“Tunamshkuru Mungu kwa Shule yetu kufanya vizuri na hizi ni jitihada za walimu kufanya kazi kwa bidii pamoja na wafunzi kuzingatia yale wanayofundishwa na walimu wao hakika zawadi hizi zimetupata faraja katika kipindi hiki kigumu tunachopitia.” Alisema Mwl. Mushi.
 Sehemu ya maonesho wakati wa Juma la Elimu lililofanyika katika viwanja wa Arusha School. 
Mgeni rasmi ambaye ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Arusha Ndg. David Mwakiposa(kwanza kushoto) akitembelea maonesho wakati wa Juma la Elimu lililofanyika katika viwanja wa Arusha School. 
Wanafunzi wa shule mbalimbali pamoja na walimu wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa sherehe za Juma la Elimu
Katibu Tawala wa Wilaya Ndg. David Mwakiposa(kushoto) akikabidhi  Kombe la Ushindi kwa kuwa nafasi ya kwanza kimkoa  kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Lucky Vicent Bw. Innocent Mushi.
Katibu Tawala wa Wilaya Ndg. David Mwakiposa(kushoto) akikabidhi cheti cha Ushindi kwa kuwa nafasi ya kwanza kiwilaya  kwa Mwl. Mkuu wa Shule ya Lucky Vicent Bw. Innocent Mushi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...