Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Kiungo mahiri wa timu ya Mbeya City Kenny  Ally amejiunga rasmi na klabu ya Singida United kwa ajili ya kuitumikia timu hiyo msimu ujao wa ligi kuu ya Tanzania bara kwa kandarasi ya miaka miwili.

Kenny ni miongoni mwa wachezaji ambao walikuwa wakiwindwa vikali na klabu kubwa za hapa nchini Simba na Yanga kila mmoja akitaka kupata saini yake ila walikuwa wakishindwana katika dau.
Usajili huo wa Kenny kwenda  Singida United ni pigo kwa timu ya Mbeya City kwani inaonekana ikiendelea kuvunjwa  kwa kusajiliwa wachezaji wao na klabu mbalimbali.

Singida United ni miongoni mwa timu ambazo zimeanza kutazamwa na wadau wa soka kwamamba huenda wakaleta mapinduzi katika soka hapa nchini hii inatokana na mipango yao ikiwemo usajili wa wachezaji wa kigeni.
 Mchezaji Kenny Ally akipokea jezi yake kutoka kwa Katibu Mkuu wa Singida United Abdulrahman Sima baada ya kukamilisha kutia saini kandarasi ya miaka miwili ya kuitumikia klabu hiyo, katikati ni  Mwenyekiti wa kamati ya Usajili wa Singida Festo Sanga.
 Mchezaji Kenny Ally akitia saini kandarasi ya miaka miwili ya kuitumikia klabu hiyo. Kulia ni  Katibu Mkuu wa Singida United Abdulrahman Sima na  Mwenyekiti wa kamati ya Usajili wa Singida Festo Sanga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...