Na Nteghenjwa Hosseah – Arusha
Mkuu wa
Wilaya ya Arusha Mhe. Gabriel Daqaro
amesema wanawake na vijana wanaokidhi vigezo wapewe Zabuni za Halmashauri ya
Jiji ili kuweza kuwainua kiuchumi na kuboresha maisha yao kwa kazi mbalimbali
zinazotolewa kila mwaka.
Daqaro
ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya wanawake na vijana ambao ni
wajasiriamali wanaonufaika na mikopo yenye riba nafuu kutoka Jiji ambayo
hutolewa kwa mujibu wa sheria.
“Ni wakati wa wanawake na vijana kuchangamkia
fursa mbalimbali katika Jiji la Arusha ikiwa ni pamoja na zabuni ambazo
zitasaidia kuinua mitaji na kuongeza pato la familia zenu, hizi kazi ni zenu
hakikisheni mnafuata taratibu zote ili mzichukue wasije watu toka mbali wakapewa
wakati ninyi ambao ni wakazi wa Mji huu mkakosa kwa kukosa vigezo vidogo
watumieni wataalamu wa Jiji wawaelimishe”amesema Daqaro.
Wakati
akisema hayo Mkuu wa Wilaya Mhe. Daqaro
amekabidhi hundi za mfano ya Tsh Mil 390 kwa vikundi vya wanawake 78 huku
vikundi vya vijana 67 vimekabidhiwa hundi ya Tsh Mil 336.
Mhe. Daqaro amesema kuwa kutokana na changamoto
iliyoko katika taasisi za fedha ambazo hutoa mikopo kwa riba kubwa na kuhitaji
dhamana ya nyumba na ardhi jambo ambalo linawakwamisha wakopaji hivyo Serikali imeamua
kutoa mikopo ya masharti nafuu ambayo ni asilimia kumi ya mapato ya ndani ya
Halmashauri.
Pia
amewasihi wanufaika wa mikopo hii kuwa mikopo itumike katika malengo maalumu na
katika miradi inatakayoleta tija kama vile uanzishwaji wa viwanda vidogo vidogo
ambavyo vitasaidia kutengeneza ajira na kukuza uchumi.
Kwa upande
wao kinamama na vijana waliopokea mikopo hiyo wamesema kuwa mikopo hiyo
itawainua kiuchumi na kuwawezesha kufanya shughuli za uzalishaji mali na
kuachana na kuwa tegemezi pamoja na matumizi ya dawa za kulevya na wizi.
Mpaka
kufikia robo ya tatu Machi 2017 Halmashauri ya jiji la Arusha imetoa mikopo ya Tsh
Bil 1.3 kwa ajili ya wanawake na
vijana kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.
Mkuu
wa Wilaya ya Arusha Mhe. Gabriel Fabian
Daqarro (katikati) akifungua mafunzo ya wajasiriamali yanayoenda sambamba
na utoaji wa mikopo ya wanawake na vijana kwa robo ya tatu.
Mkurugezi
wa Jiji la Arusha Ndg. Athumani Kihamia
(tatu kulia) akizungumza kwenye ufunguzi wa mafunzo kwa wajasiriamali ambao ni
wanufaika wa mikopo ya Halmashauri ya Jiji kwa robo ya tatu.
Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Gabriel Fabian Daqarro (katikati)
akiwakabidhi hundi ya mfano ya Tsh Mil 390 kwa vikundi vya wanawake Jiji la
Arusha.
Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Gabriel Fabian Daqarro (katikati)
akikabidhi hundi ya mfano ya Tsh Mil 336 kwa vikundi vya vijana, Jiji la
Arusha.
Washiriki
wakifuatilia mafunzo ya ujasiriamali kabla ya kukabidhiwa mikopo ya riba nafuu toka
Jiji la Arusha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...