Jovina Bujulu-MAELEZO.

Tanzania ni miongoni mwa nchi 193 zilizosaini mkataba wa Umoja wa Mataifa wa kupambana na kuenea hali ya jangwa duniani (UNCCD). Mkataba huu unalenga kupambana na tatizo la uharibifu wa ardhi katika maeneo yenye ukame na kufanya juhudi za kuyahifadhi.

Mkataba huu ni muhimu kwa nchi yetu ambayo uchumi wake unategemea ardhi kwa ajili ya kilimo ambacho kinachochea maendeleo na ajira kwa wananchi walio wengi.

Hivi karibuni dunia iliadhimisha siku ya kupambana na kuenea kwa hali ya jangwa na ukame ambayo ilikiongozwa na kauli mbiu isemayo “Ardhi ni makazi yetu tuitunze kwa manufaa ya baadaye”. Kauli mbiu hii inahamasisha jamii kutunza ardhi kwa kuwa ndiyo makazi yetu.

Akiongea hivi karibuni mjini Dodoma, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba alisema kuwa kauli mbiu hii inahimiza jamii kuongeza juhudi za kutunza ardhi, na kuzingatia maendeleo endelevu ya rasilimali tulizo nazo kwa ajili ya maendeleo ya sasa na kwa vizazi vijavyo.

Madhumuni ya kuadhimisha siku hii ni pamoja na kuongeza uelewa miongoni mwa jamii na kujua athari za jangwa na ukame katika maisha ya kila siku ya binadamu na jinsi ya kuthibiti hali hiyo.

“Malengo hayo yanadhihirisha umuhimu wa utunzaji wa ardhi na udongo kwa matumizi endelevu hasa kwa ajili ya kilimo, mifugo, na huduma nyingine kama utalii wa wanyama pori na uwindaji.” Aliongeza Mhe. Makamba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...