Mashauri 18 ya madai ya kodi ya ardhi yenye thamani ya shilingi bilioni 1.1 yamewasilishwa katika Baraza  la ardhi na nyumba  wilaya ya Tanga ikiwa ni mkakati wa Serikali wa kuwabana wamiliki wa viwanja wanao kwepa kulipa kodi.
Akizungumza mara baada ya kuwasilishwa kwa mashuari hayo mwakilishi wa afisa ardhi msaidizi kanda ya kazikazini Thadeus Riziki amesema hatua ya kuwafikisha mahakamani wamiliki wa viwanja  hivyo ni kupata kibali kitakacho wezesha wizara kulipwa makusanyo ya madeni.
Amesema baada ya halmashauri kuwapelekea wamiliki hati ya madai na kushindwa kulipa hatua inayofuata ni kuwafikisha mahakamani ili kupata ridhaa ya kisheria ya kukamata mali za wadaiwa.
Kwa upande wake afisa ardhi mteule Halmashauri ya jiji  la Tanga Straton Thobias amesema katika mwaka wa fedha wa 2016/7 halmashauri imeweka lengo la  kukusanya kodi ya ardhi kiasi cha shilingi bilioni 2.5 ambapo hadi sasaimefanikiwa kukusanya shilingi bilioni 2.3
Akizungumzia zoezi hilo mwanasheria ofisi ya kamishina wa ardhi  Rosemery Mshana amesema wamiliki wa ardhi wanatakiwa kilipa kodi bila shuruti na kwamba kinyume chake watafikishwa mahakamani  mujibu wa kifungu cha  50  cha sheria ardhi namba nne(4). H
abari kwa hisani ya blog ya Kijamii ya Tanga Raha.
Mwakilishi wa Kamishna wa Ardhi Msaidizi Kanda ya
Kaskazini, Ardhi Mwandamizi Thadeus Riziki akizungumza na
waandishi wa habari kuhusu Baraza la Ardhi Mkoani Tanga kupokea mashauri 18 yenye thamani ya Bilon 1.1 ambayo yamefikishwa kutokana wamiliki wa nyumba ,makazi na viwanda  kushindwa kulipa kodi ya ardhi kwa wakati

 Afisa Ardhi Mteule Halmashauri ya jiji  la Tanga Straton Thobias akielezra mkakati wa  mwaka wa fedha wa 2016/7 halmashauri imeweka lengo la  kukusanya kodi ya ardhi kiasi cha shilingi bilioni 2.5 ambapo hadi sasaimefanikiwa kukusanya shilingi bilioni 2.3
Mwanasheria wa  Ofisi ya Kamishina wa Ardhi Kanda ya Kaskazini  Rosemery Mshana akiwataka wamiliki wa ardhi wanatakiwa kilipa kodi bila shuruti na kwamba kinyume chake watafikishwa mahakamani  mujibu wa kifungu cha  50  cha sheria ardhi namba 4.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...