Muonekano wa picha kwenye Tamasha la Kids Circus Carnival. Benki ya NMB ilikuwa ni mmoja wa makampuni wadhamini.

BENKI ya NMB Tanzania jana iliungana na Watanzania nchini kusherehekea Siku Kuu ya Eid El Fitr kwa kuwa mmoja wa makampuni wadhamini wa tamasha lililoandaliwa na kampuni ya Azam la Kids Circus Carnival ambalo limehusisha watu wa aina mbalimbali kuanzia watoto na hata watu wazima kufurahi kwa pamoja. 

Tamasha hilo ambalo linafanyika kwa siku mbili mfululizo yaani Eid Mosi (Juni, 26) na Eid Pili (Juni, 27) linafanyika katika viwanja vya Kenyatta (Kenyatta Ground) vilivyopo Osterbay, jijini Dar es Salaam. 

Katika tamasha hilo lililokuwa na michezo anuai lilijumuisha huduma mbalimbali ambazo zinazotolewa na Benki ya NMB ambapo watu waliohudhuria tamasha walipata nafasi ya kujua huduma zinazotolewa na NMB, na pia kupata nafasi ya kufungua akaunti. 

Pamoja na hilo pia kulikuwa na michezo mbalimbali ya watoto na maonesho ya wanyama mbalimbali wakiwepo simba, chui, mamba, farasi, sungura na wengine wengi. Zifuatazo ni picha mbalimbali za tamasha hilo. Watoto mbalimbali wakifurahia huduma kwenye Tamasha la Kids Circus Carnival.
Watu mbalimbali wakifurahia huduma kwenye Tamasha la Kids Circus Carnival Watoto mbalimbali wakifurahia huduma kwenye Tamasha la Kids Circus Carnival. Baadhi ya michezo kwenye Tamasha la Kids Circus Carnival.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...