IDARA ya Uhamiaji Mkoani Tanga imeanza mikakati ya kukabiliana kwa vitendo na wimbi la wahamiaji haramu kuingia mkoani hapa kwa kuanzisha kizuizi eneo la Mkata wilayani Handeni kwa muda wa saa 24. 

Hayo yalibainishwa na Afisa Uhamiaji Mkoani Tanga DCI, Crispin Ngonyani wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mipango waliojiwekea kuzibiti vitendo vya namna hiyo. 

Alisema wameamua kuanzisha mpango huo kutokana na asilimia kubwa ya wahamiaji haramu hao wanapokuwa wamefika kwenye eneo hilo la kizuizi wanashushwa na kupakia pikipiki maarufu kama bodaboda na kuingia mkoani Tanga. 

“Kutokana na hali hiyo ndio maana tumeamua kuweka kizuizi hicho ambacho kimekuwa ni eneo ambalo linatumika kuwafaulisha wahamiaji haramu kwenye pikipiki maarufu kama bodaboda kwa lengo la kuzibiti suala hilo kwa vitendo “Alisema. 

Aidha pia alisema hivi sasa wamejipanga kuhakikisha wanadhibiti maeneo yote ambayo yamekuwa na mianya ya kutumia kwa ajili ya kupitia ili kuweza kuhakikisha hawaingii mkoani Tanga. 

“Lakini pia tuwatake wananchi kuhakikisha wanawafichua wahamiaji haramu pindi wanapokuwa wakiwaona kwenye maeneo yao kwani wamekuwa na madhara makubwa hivyo wanapaswa kutoa taarifa kwa mamlaka husika “Alisema. 

Hata hivyo aliwataka wananchi kuendelea kutoa taarifa iwapo watabaini kuwepo kwa watu wasiowaelewa kwenye maeneo yao ili hatua kali ziweze kuchukuliwa.


Habari kwa hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...