NA WAMJW –DAR ES SALAAM.

CHANJO ya homa ya Ini inatarajiwa kupatikana kwa wananchi wote bila kujali kigezo cha umri wala uwezo wa kifedha kwa wananchi wenye hatari au ugonjwa wa ini kwa bei nafuu mpaka kufikia mwaka 2020 kutoka mwaka wa fedha 2018/2019.

Hayo yamezungumzwa na Waziri wa afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia , Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es salaam kuhusu maadhimisho ya ugonjwa wa homa ya ini duniani.

“Katika kuadhimisha siku ya ugonjwa wa homa ya ini duniani tumedhamiria kuhakikisha chanjo ya ugonjwa huu inapatikana kwa watu wote nchini ambao wana hatari ya kupata maambukizi ya homa ya ini au tayari wamepata ugonjwa huo kwa bei nafuu kwa mswaka wa bajeti 2018/2019” alisema Waziri Ummy. 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiwahutubia waandishi nwa habari (Hawapo kwenye picha) katika kilele cha maazimisho ya siku ya Homa ya Ini Duniani yaliyofanyika leo katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mganga mkuu wa Serikali Pro Muhamad Bakari kambi na Kulia ni Afisa kutoka kitengo cha magonjwa ya Mlipuko Dkt. Azma Simba. 
Waandishi wa habari kutoka vyombo tofauti wakifuatilia kwa ukaribu tamko la kilele cha maadhimisho ya Homa ya Ini Duniani lililotolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu (Hayupo kwenye picha) leo katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...