Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

WATANI wa jadi Simba na Yanga watakutana Agosti 23 katika mchezo wa ngao ya hisani ikiashiria ufunguzi msimu mpya wa ligi kuu ya Vodacom 2017/18.

Pazia rasmi la ligi hiyo litafunguliwa Agosti 26 ambapo mechi saba zitachezwa katika viwanja mbalimbali nchini ambapo itamalizika Mei 20 mwakani kwa kupatikana bingwa mpya.

Ofisa Habari wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) amewaambia Waandishi wa Habari kuwa mchezo huo wenye kuvuta hisia za mashabiki wengi ndani na nje ya nchi utafanyika kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

"Mchezo wa ngao ya hisani kati ya Simba na Yanga utafanyika Agosti 23 kwenye uwanja wa Taifa ukiashiria kuanza kwa msimu mpya wa ligi 2017/18 na wiki moja mbele itaanza rasmi," alisema Lucas.

Aidha Lucas amesema miamba hiyo itakutana tena Oktoba 14 katika mchezo wa kwanza wa msimu kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa.

Ratiba ya michezo katika wiki ya kwanza ya ligi hiyo.

Agosti 26
Ndanda vs Azam FC
Mwadui FC vs Singida United
Mtibwa Sugar vs Stand United
Simba vs Ruvu Shooting
Kagera vs Mbao FC
Njombe Mji vs Prisons
Mbeya City vs Majimaji

Agosti 27
Yanga vs Lipuli.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...