Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akiweka saini kwenye kitabu cha wageni wakati alipowasili katika ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Antony Mtaka, kwa lengo la kujitambulisha kwenye Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa huo, IGP Sirro yupo mkoani humo kwa ziara ya kikazi na kuzungumza na askari wa Jeshi hilo.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Antony Mtaka (kushoto), akimsikiliza Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, ambaye amefika katika ofisi yake kwa lengo la kujitambulisha kwenye Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa huo, IGP Sirro yupo mkoani humo kwa ziara ya kikazi na kuzungumza na askari wa Jeshi hilo, kulia ni kamanda wa Polisi mkoa wa Simiyu, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Boniveture Mushongi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akizungumza na baadhi ya wananchi wa Mwamapalala mkoani Simiyu, wakati akiwa njiani kuelekea mkoani Shinyanga, kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kuzungumza na askari wa Jeshi hilo pamoja nakujua changamoto wanazokutananazo wakitekeleza majukumu yao.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akizungumza na baadhi ya wananchi wa Maganzo mkoani Shinyanga, wakati alipowasili akitokea mkoani Simiyu kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kuzungumza na askari wa Jeshi hilo pamoja nakujua changamoto wanazokutananazo wakitekeleza majukumu. Picha na Demetrius Njimbwi – Jeshi la Polisi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...