Na Mwene Said wa Blogu ya Jamii, Dar es Salaam.

Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, imeupa muda wa siku tano kuwasilisha pingamizi la awali dhidi ya maombi ya dhamana ya kesi ya  uhujumu uchumi inayomkabili  Mfanyabiashara Yusufali Maji (41) na wenzake watatu.

Manji na wenzake, pia wanakabiliwa na  kukutwa na vitambaa vya sare za Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ)  isilivyo halali vyote vikiwa na thamani ya Sh. milioni 236.5.

Hata hivyo, mfanyabiashara huyo amefungua maombi yaliyosajiliwa kwa namba 122/2017, kupinga hati iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) kuzuia dhamana dhidi yake na yalitajwa jana mbele ya Jaji Isaya Arufani.

Upande wa mashtaka ukiongozwa na Paul Kadushi, Simon Wankyo na Tulumanywa Majigo, ulidai mahakamani kwamba wanaomba muda kwa sababu wana nia ya kuwasilisha pingamizi la kupinga maombi ya utetezi.

Pia, ulidai kuwa wanaomba mahakama iwape muda wa kuwasilisha majibu ya hati ya maombi ya mshtakiwa.

Jaji Arufani alisema upande wa Jamhuri uwasilishe majibu na pingamizi lao Agosti Mosi na upande wa utetezi kama watakuwa na majibu ya nyongeza wawasilishe Agosti 2 na mahakama hiyo itasikiliza maombi hayo Agosti 4, mwaka huu.
Katika maombi hayo,  Manji anaiomba Mahakama Kuu kutengua hati ya DPP ya kuzuia dhamana yake  iliyowasilishwa Julai 5, mwaka huu aliposomewa mashtaka ya uhujumu uchumi ikiwamo kukutwa na sare hizo.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...