Watanzania wametakiwa kutumia fursa zinazoendelea kuwekwa na serikali ya awamu ya tano kujikita katika ujasiriamali na kuanzisha viwanda kwa ajili ya kujenga uchumi viwanda ili kufikia uchumi kati na kuboresha ustawi wa jamii hapa nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji,Profesa Adolf Mkenda alisema hayo wakati wa mkutano wa wadau uliokuwa ukijadili rasimu ya mapendekezo ya kuwa na mkakati wa kitaifa kuendeleza ujasiriamali hapa nchini, kuwa wakati wa watanzania kujikita katika ujasiriamali na kuwekeza katika viwanda umewadia.

“Wakati wa watanzania kuanzisha viwanda kuzalisha bidhaa zinazotokana na mali ghafi za hapa nchini umewadia,” na hakuna wakati mzuri zaidi kuliko kipindi hiki ambacho serikali imweka kipaumbele zaidi katika hili, aliongeza kusema Profesa Mkenda.

Mkakati huo wa kitaifa wa kuendeleza ujasiriamali umeandaliwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali likiwemo Shirika la Umoja wa Mataifa Linalojihusisha na Maendeleo ya Biashara (UNCTAD).
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji,Profesa Adolf Mkenda (katikati) akifuatilia mada iliyokuwa inatolewa na Mwezeshaji, Dkt Donath Olomi hayupo pichani wakati wa mkutano wa wadau uliokuwa ukijadili rasimu ya mapendekezo ya kuwa na mkakati wa kitaifa kuendeleza ujasiriamali hapa nchini, wapili kushoto Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC),Bi. Beng’I Issa, kushoto ni Mwakilishi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa Linalojihusisha na Maendeleo ya Biashara (UNCTAD),Bw. Lorenzo Tosini, wa pili kuli ni Mkurugenzi Msaidizi Mazingira ya Biashara Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Christopher Mramba na kulia ni Mkurugenzi wa Uwezeshaji wa baraza hilo, Bi. Anna Dominick.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji,Profesa Adolf Mkenda (katikati) akiteta jambo na Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC),Bi. Beng’I Issa, wakati wa mkutano wa wadau uliokuwa ukijadili rasimu ya mapendekezo ya kuwa na mkakati wa kitaifa kuendeleza ujasiriamali hapa nchini, na kulia ni Mwakilishi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa Linalojihusisha na Maendeleo ya Biashara (UNCTAD),Bw. Lorenzo Tosini.


Wadau kutoka taasisi mbalimbali wakiwa katika makundi wakati wa mkutano uliokuwa ukijadili rasimu ya mapendekezo ya kuwa na mkakati wa kitaifa wa kuendeleza ujasiriamali hapa nchini, aliyesimama ni mwezeshaji wa mkutano huo, Dkt. Donath Olomi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...