Harakati za ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Mao Tse Tung uliopo Mpirani Kikwajuni Mjini Zanzibar zinaendelea karibu Miezi Miwili sasa chini ya Wahandisi wa Kampuni ya Kimataifa ya Zhengtai Group ya Jamuhuri ya Watu wa China.


Ujenzi huo unafuatia msada mkubwa ulioidhinishwa na Serikali ya Jamuhuri ya Watu wa China kwa Serikali ya Zanzibar katika azma ya kuimarisha uhusiano wa muda mrefu wa pande hizo mbili ukizingatia heshima uliopewa Uwanja huo wa kuitwa jina la Muasisiwa Taifa la China Hayati Mao Tse Tung.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipata fursa ya kutembelea Uwanja huo kujionea harakati za ujenzi huo kazi ambayo inaonyesha mafanikio mazuri.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akitembelea harakati za ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Mao Tse Tung uliopo Mpirani Kikwajuni Mjini Zanzibar. Kushoto ya Balozi Seif ni Waziri wa Hbari, Utamaduni, Utalii na Michezo Rashid Ali Juma.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Omar Hassan Omar akimuonyesha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif hayupo pichani ramani ya Uwanja wa Mao Tse Tung utakavyokuwa baada ya kukamilika kwake.
Balozi Seif katika picha ya pamoja na Uongozi wa ngzi ya juu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo pamoja na wahandisi wa nujenzi wa uwanja wa michezo wa Mao Tse Tung.


Balozi Seif akiagana na Mshauri wa Rais wa Zanzibar katika masuala ya Utamaduni Chimbeni Kheir baada ya kuangalia harakati za ujenzi wa uwanja wa michezo wa Mao hapo Mpirani Kikwajuni Mjini Zanzibar.  Picha na – OMPR – ZNZ.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...