Rais mstaafu wa awamu ya nne ,Dk.Jakaya Kikwete,akionyesha Kilimo cha mahindi ya njano kwa ajili ya kuongeza rutuba kwa ng'ombe .
Rais mstaafu wa awamu ya nne ,Dk.Jakaya Kikwete,akionyesha eneo analohifadhi majani ya malisho ng'ombe .
RAIS Mstaafu wa awamu ya nne ,Dk.Jakaya Kikwete ,amesema ameanza kufanya kilimo na ufugaji tangu mwaka 1988/1989 hivyo anaetegemea kufanya shughuli hizo baada ya ustaafu amechelea .
Aidha ameeleza matarajio yake kwa sasa ni kuongeza mifugo ya ng'ombe majike wa maziwa 500 watakaoweza kutoa maziwa lita 2,000 hadi 4,000 kwa siku .
Katika hatua nyingine dk.Kikwete amesema endapo wafugaji watazingati ufugaji wa kisasa kwa kuwa na maji ya kutosha ,malisho ,kinga ya chanjo na kuogeshwa ni lazima watanufaika kwa kupata soko la uhakika hasa maziwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...