WAMJW- Rukwa

Manispaa ya Sumbawanga imeelekezwa kuongeza kujenga vituo vya afya kulingana na jiografia ilivyo ili hospitali ya Rufaa ya mkoa ibaki kutoa huduma za kibingwa mkoani hapa.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati akiongea na watumishi wa sekta ya afya wa Mkoa na Wilaya kwenye ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wakati wa majumuisho ya ziara ya siku mbili ya kikazi

Alisema Serikali inaboresha hospitali za Rufaa za Mkoa kwa ajili ya huduma za kibingwa hivyo hospitali hizo ziweze hutoa huduma za kimatibabu ya kibingwa hasa kwa watu wenye huitaji huo,”lakini wananchi wanapaswa kufuata utaratibu wa sera unavyosema kwenda kupata matibabu katika hospitali za Rufaa ni lazima mgonjwa aandikiwe rufaa na sio kila mtu anaenda moja kwa moja kwenye hospitali hizo”

Waziri Ummy alisema kulingana na kuboresha utoaji wa huduma za afya nchini ni vyema na mkoa kwa ujumla ni vyema kujenga vituo hivyo vitakavyoweza kutoa huduma kwa wananchi waliopo maeneo husika kuliko kujenga hospitali ya Wilaya ambayo wananchi waliopo maeneo ya mbali wapate huduma za afya huko huko karibu na huduma hizo ziwe bora.

“Fanyeni maamuzi yenye manufaa kwa wananchi wa wilaya yenu ili muwasogezee huduma watu wenu,alisema kwa Wilaya ya Nkasi wao wanatakiwa kujenga hospitali ya wilaya ya serikali ambapo Wizara yake itasaidia kutoa milioni 350 kati ya 650 ambayo itajenga wodi ya wazazi,maabara pamoja na nyumba moja ya mtumishi
Waziri wa Afya Ummy Mealimu akiongea na mmoja wa wagonjwa waliofika kupata matibabu kwenye kituo cha afya cha Mazwi kilichopo Manispaa ya Sumbawanga

Waziri Ummy mwalimu akimuuliza mmoja wa mama aliyefika kupata matibabu ya nje kwenye kituo cha afya cha Mazwi kama amefika muda mrefu na hajapata matibabu,waziri huyo yupo mkoani Rukwa kwa ajili ya ziara ya kikazi ya kukagua huduma za afya zinazotolewa kwenye vituo vya huduma nchini
Waziri Ummy Mwalimu akiongea na mama mjamzito aliyelazwa kwenye Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Rukwa.Waziri Ummy alisisitiza watoa huduma kuhakikisha awatoa huduma wa afya wanajitahidi kuepusha vifo vianavyoweka kuepukika kutokana na uzazi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...