Ujumbe wa wabunge watano wa Bunge la Congress la Marekani wakiangalia ngoma za asili mara baada ya kuwasili kwenye ofisi za Shirika la Vijana Tayoa Bahari Beach Dar es Salaam.

 Kaimu Balozi wa Marekani Dk. Inmi Patterson akisailimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Vijana Tayoa, Balozi Charles Sanga alipowasili kwenye viwanja vya shirika hilo Bahari Beach Dar es Salaam pamoja na ujumbe wa wabunge watano wa Bunge la Congress la Marekani.
 Kaimu Balozi wa Marekani,  Dk. Inmi Patterson, wa kwanza kushoto akifurahia jambo na ujumbe wa wabunge watano wa Bunge la Congress la Marekani wakati wanazindua redio ya kuelimisha vijana kuhusu mbalimbali kwenye Shirika la Vijana Nchini Tayoa. Wapili kulia ni Mkurugenzi wa Tayoa Peter Masika.

Na Mwandishi Wetu
UBALOZI wa Marekani nchini, umesifu kazi zinazofanywa na Shirika la Vijana Nchini (Tayoa), katika kuwainua na kuwahamasiha vijana kujikwamua kiuchumi na kushiriki kwenye shughuli mbalimbali za maendeleo nchini.

Hayo yalisemwa jana na Kaimu Balozi wa Marekani nchini, Dk. Inmi Patterson, wakati ujumbe wa wabunge watano wa Bunge la Congress la Marekani wakiwa na familia zao, ulipotembelea ofisi za Shirika hilo zilizoko Bahari Beach, jijini Dar es Salaam.

Wabunge hao wa Congress walioambatana na Kaimu Balozi wa nchi hiyo ni pamoja na Carly Paul, Bob Goodlatte, Steve King, Blake Farenthold, Mike Bishop na Sheila Jackson Lee.

 Wabunge hao walijionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na Shirika hilo ikiwemo elimu ya bure kuhusu masuala ya Ukimwi kupitia simu za bure, ujasiriamali na miradi mbalimbali ya kuinua vijana.

Balozi alisema yeye na ujumbe wake wamefurahi kuona kazi kubwa zinazofanywa na Tayoa kwa kushirikiana na taasisi za Marekani kama Kituo cha Kudhibiti Maradhi cha Center for Disease Control (CDC).

“Tumefurahi sana kuona kazi zenu na hasa mnavyowashirikisha vijana katika kujikwamua kiuchumi na kutafuta maendeleo, nawapongeza sana Tayoa kwa kazi kubwa mnayofanya,” alisema

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...