Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma, Mheshimiwa Jaji (Mstaafu) Dkt. Steven J. Bwana (pichani) amewataka watumishi wa umma kuhakikisha wanafanya kazi kwa uadilifu na kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za Utumishi wa Umma na kujiepusha na vitendo vya rushwa kwenye utekelezaji wa majukumu yao.

Akizungumza katika mahojiano maalum hivi karibuni, Dkt. Bwana amesema Tume katika kutekeleza majukumu yake ya msingi ya ukaguzi wa rasilimali watu na kushughulikia rufaa na malalamiko, imebaini kuwepo kwa ukiukwaji wa Sheria, Kanuni na Taratibu miongoni mwa Watumishi wa umma, Waajiri, Mamlaka za Ajira na Nidhamu.

Amesema kuwa baadhi ya Watendaji Wakuu wanashindwa kuwachukulia hatua kwa mujibu wa Sheria, watumishi wenye utendaji usioridhisha na wanaokiuka maadili ya utumishi wa umma walio chini yao. Tatizo hili lipo zaidi kwa baadhi ya Halmashauri zetu na Taasisi za Umma.

“Kumekuwa na udhaifu mkubwa kwa baadhi ya Watendaji Wakuu ambao wameshindwa kuchukua hatua za nidhamu mapema dhidi ya watumishi walio chini yao. Utakuta mtumishi anatoweka tu kazini bila kutoa taarifa wala kuomba ruhusa! Mtumishi kutokuwepo kazini kwa siku tano bila ruhusa wala sababu za msingi adhabu yake ni kufukuzwa kazi. Inashangaza kuona mtumishi wa umma hayupo katika kituo chake cha kazi kwa zaidi ya siku tano, siku 115 na Mwajiri wake hajui, wala hachukui hatua.” Amesema.

Hata hivyo, Dkt. Bwana ameonyesha kutoridhishwa na hali ya utendaji kazi katika baadhi ya Halmashauri. Alisema, “Rufani nyingi tunazopata zinatoka huko, kuna haja ya kurekebisha mambo mengi sana hasa kwenye Halmashauri zetu, hakuko sawa kwa upande wa usimamizi wa Rasilimali watu. Kuna wizi kule, kuna matumizi mabaya ya fedha za umma na mali za Halmashauri.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...