Na Karama Kenyunko, Glogu ya jamii.

WAFANYABIASHARA wawili  wakazi wa Kimara jijini Dar es Salaam, Jumbo Cheto(39)  na  Anna Kilawe (43) leo wamepandishwa katika kizimba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka ya wizi wa mafuta ya mawese na sabuni zenye thamani ya milioni 60.

Hati ya mashtaka imesomwa na  wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi ambae amedai siku na mahali pasipojulikana, wote wawili walikula njama ya wizi iloyokuwa safarini.

Imedaiwa, kati ya Mei 19 na 23, mwaka huu,  huko kinondoni washtakiwa hao waliiba magaloni 1056 za mafuta ya mawese ya Lita 20, madumu mengine ya Lita 200 na sabuni 1319 ambapo vitu vyote vina thamani shilingi milioni 60.

Washtakiwa wamekana mashtaka hayo na kwai hiyo itatajwa tena Agosti 30, mwaka huu.
Mfanyabiashara, Jumbo Cheto(39) mkazi wa Kimara jijini Dar es Salaam
amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashtaka ya wizi wa mafuta ya mawese na sabuni zenye thamani ya milioni 60.
 Mfanyabiashara,  Anna Kilawe (43) mkazi wa Kimara jijini Dar es Salaam (Mwenye nguo ya Pink) amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashtaka ya wizi wa mafuta ya mawese na sabuni zenye thamani ya milioni 60.
Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...