Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James, akipokea mfano wa hundi ya shilingi bilioni 19.5 kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Ally Laay, ikiwa ni gawio kutokana na hisa zinazomilikiwa na serikali katika benki hiyo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla ya kupokea mfano wa hundi ya shilingi bilioni 19.5 kutoka Benki ya CRDB, ikiwa ni gawio kutokana na hisa zinazomilikiwa na serikali katika benki hiyo. Hafla hiyo imefanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Hazina, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Ally Laay akifuatiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akifafanua jambo, wakati wa hafla ya kupokea mfano wa hundi ya shilingi bilioni 19.5 kutoka Benki ya CRDB, ikiwa ni gawio kutokana na hisa zinazomilikiwa na serikali katika benki hiyo. Hafla hiyo imefanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Hazina, jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Ally Laay.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...