Na Agness Francis, Blogu ya jamii
 SSERIKALI ya Tanzania wakishirikiana na serikali ya Korea Kusini  wamezindua utekeleza mradi utakaosaidia kuboresha  upatiikanaji wa  huduma bora  za ardhi  katika mkoa  wa Mwanza  na mradi huo  utanzia Manispaa ya Ilemela na Nyamagana.

Ambapo  hafla hiyo ya mradi huo umezinduliwa leo na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,  Dkt Angeline Mabula  katika ukumbi wa  Hyatt Regency hoteli Jijini  Dar es Salaam.   

Katika ushirikiano huo wa kuimarisha utawala wa ardhi nchini ambapo makubaliano rasmi  ya ushirikiano huo yalianza mwaka 2015, ikiwa ni msada wa vifaa vya upimaji na mafunzo yanayohusu  matumizi ya vifaa vya kisasa vya upimaji, nayo yalianza mwaka 2016.

Naibu waziri Angeline Mabula ametamabaisha kuwa kuleta teknolojia hiyo mpya na nafuu  itarahisishia serikali  upimaji ardhi kwa kupanga na kupima kila kipande, pamoja na kusaidia wananchi kupata kumbukumbu na taarifa za ardhi kwa urahisi.

Mbali na hayo Dkt Angeline Mabula  ametoa shukrani za dhati kwa Serikali ya Korea Kusini kwa kuona umuhimu wa utekelezaji wa mradi  huo ambao utaleta mapinduzi makubwa  katika sekta ya ardhi hapa nchini.
 Balozi wa Korea Kusini Tanzania, Song Geum-Young  akizungumza na mkurugenzi halmashauri ya Manispaa Ilemela pamoja na wakuu wa idara na taasisi wizara ya ardhi kuhusu ushirikiano uliopo kati ya Serikali ya Tanzania na Korea Kusini kuimarisha mfumo bora wa upimaji ardhi kwa urahisi.leo katika uzinduzi uliofanyika kwenye ukumbi Hayyat Regency Hotel Jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa biashara  wa Kampuni ya LX, Cho Man-Seung akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusu kuwa mradi huo unatarajia kuanza kutekeleza  hivi karibuni na  utakuwa ni wa kisasa zaidi hapa Nchini.
 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Dkt Angeline Mabula akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa maradi wa uboreshaji wa huduma za ardhi leo  uliofanyika kwenye ukumbi wa Hayyat Regency Hotel Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wageni waalikwa pamoja na wakuu wa idara na taasisi wizara ya ardhi waliohudhuria uzinduzi huo leo katika ukumbi Hayyat Regency Hotel Jijini Dar es Salaam. (Picha na Agness Francis, Blogu ya Jamii)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...