Uwanja wa Majimaji Songea.

Na. Honorius Mpangala.

BADO sijafanikiwa kupata majibu na kujua ni nini wanachopewa kamati ya ukaguzi wa viwanja vinavyotumika ligi kuu. Yawezekana kuna mazingira ambayo yanafanyika ili kuweza kuruhusu viwanja kama wa Majimaji Songea kutumika ligi kuu. Januari 2017 katika moja ya makala zangu iliyohusu Viwanja niliandika mengi kuhusu viwanja visivyowatendea haki wachezaji wetu. Na katika hilo moja kwa moja huwezi kupindisha kulielekeza TFF kama wadau namba moja ndipo baadae liende kwa Wamiliki wa Uwanja.

Nashukuru makala ile nilipata ujumbe mwingi wa simu kutoka maeneo mbalimbali. Hatimaye Uwanja wa Namfua uliokuwa kama picha katika makala ile unarekebishwa. Niliandika kuhusu Namfua ikiwa daraja la kwanza na inapambana kupanda ligi kuu. Watu wa Singida kwa namna moja au nyingine naweza kusema walinisoma na walinielewa kwa sababu Uwanja wao ilikuwa sehemu ya kufungia mifugo kama mbuzi na ng'ombe.

 Shirikisho kuendelea kuwaheshimu watazamaji na kuwanyima raha wale wanaotazamwa uwanjani ni jambo linalosikitisha. Hata ikitokea kama tuna malengo makubwa ya kulifanya soka letu lichezwe maeno mengi  ya nchi basi tuna kazi ya kubadili mitazamo ya viongozi wetu kwa kiasi kikubwa. 

Uchaguzi mkuu wa TFF umefanya lile rungu la kufungia viwanja baada ya kukaguliwa lisifanye kazi kwasababu ya hofu ya kupunguza kura. Ikiwa tunaelekea kwenye uchaguzi wa shirikisho vifungo kadhaa vilifunguliwa kwa wale waliofungiwa. Hapo ndipo hali ya kiutendaji kwa wakati ule ilipokuwa ya kusaka kura zaidi kuliko kusimamia kwa weledi mambo ya yanayohusu soka.

Ni aibu kuona uwanja kama wa Majimaji ambao msimu wa tatu mfululizo Tangu timu ilipopanda Mara ya mwisho 2015 kuwa na nyasi zile. Kila msimu kamera za Azam TV zinapokuwa katika uwanja wa huo unasikitika mtazamaji. Viko vibanda umiza ambavyo wamiliki hufikia hatua ya kusema mechi ya Majimaji msilipe kiingilio maana inachezwa Kwenye jaruba lililotoka kuvunwa mpunga hivi punde. Kiuhalisia huwezi kutofautisha kati ya majaruba ya shamba la Nafco Kapunga kule Mbarali Mbeya na eneo la kuchezea la uwanja wa Majimaji. Halafu unakuta chama cha soka eneo hilo kinajinasibu kufanya vyema katika utawala wao. Unaweza kujiukiza maswali mengi kuwa mgawanyo wa mapato kwa wamiliki na chama cha soka yanatumika ipasavyo au ni kama shamba la miwa karibu na shule msingi.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...