Waomboleaji wakiwemo ndugu,jamaa na marafiki wakiwa wamebeba jeneza ambalo lina mwili wa Kaka yake Mufti wa Tanzania,Shekhe Saad Zubeiry Ally ambaye amefariki katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam wakijiandaa kuliingiza kaburini wakati wa mazishi yaliyofanyika jana (Septemba 21) kwenye makaburi ya familia eneo la Kwamndolwa wilayani Korogwe Mkoani Tanga.
Mufti wa Tanzania Shekhe Aboubakar Zubeir katika akizungumza wakati wa mazishi hayo yaliyofanyika katika eneo la Kwamndolwa wilayani Korogwe Mkoani Tanga.
Mufti wa Tanzania Shekhe Aboubakar Zubeir kulia akiteta jambo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu wakati wa maziko ya kaka yake Mufti yaliyofanyika kwenye eneo la Makaburi ya familia eneo la Kwamndolwa wilayani Korogwe kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini (CCM) Marry Chatanda.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu kushoto akiteta jambo na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira,January Makamba wakati wa maziko hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...