Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Martine Shigella, akipokea msaada wa vifaa tiba kutoka kwa Mwenyekiti wa UZALENDO KWANZA, Steve Nyerere wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa tiba iliyofanyika katika viwanja vya Tanga Manno mapema jana mjini Tanga. PICHA ZOTE NA KAJUNASON/MMG - TANGA.
Vifaa vilivyotolewa na wasanii na wachezaji hao katika uwanja wa Tangamano ikiwa ni Kampeni ya Uzalendo kwanza ni pamoja na Ultra Sound, mashine ya X- Ray, Wheel Chair, Magongo ya walemavu na craches.
Shigella amepokea vifaa hivyo ikiwa ni moja ya Kampeni ya UZALENDO KWANZA ambayo inaongozwa na wasanii na wacheza mpira ikiwa na lengo la kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika kuchangia maendeleo ya nchi. Ambapo vifaa hivyo vinagawiwa katika hospitali za Ngamiani, Makorola, Pongwe na Mikanjuni.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Martine Shigella, akitokea msaada wa vifaa tiba kutoka kwa Mwenyekiti wa UZALENDO KWANZA, Steve Nyerere wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa tiba iliyofanyika katika viwanja vya Tanga Manno mjini Tanga.
Vijana wazalendo wa UZALENDO KWANZA wakibeba vifaa Tiba ambavyo walitoa kwa ajili ya hospitali za mkoa wa Tanga.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...