Na Agness Francis Blogu ya jamii.

Katika tamasha la tamasha la muziki Mnene lililokonga nyoyo za mashabiki  ambalo limefanyika  katika ukumbi wa New Msasani Jijini Dar es Salaam  ambapo wasanii kama Chidi Benzi, Nuhu Mziwanda, Izzo Business, Bob Junior, Makomando pamoja na Kayumba Asosiye  mshindi wa BSS walitoa burudani ya kutosha  kwa wakazi hao wa Kinondoni.

Hata hivyo Michuzi Blog imezungumza na msanii Kayumba Asosiyee ambaye mpaka hivi sasa yupo chini ya meneja wake Mkubwa Fella ametanabaisha kuwa kuwepo kwa tamasha  hilo la Mziki nene linasaidia kukuza  vipaji vya wasanii chipukizi vilivyolala.

Vile vile msanii huyo amesema  kuwa changamoto ya muziki wa sasa mchuano umekuwa mkali sana kwa sababu mashabiki wanajua muziki mzuri, inabidi kupambana ili kuhakikisha unatoa kitu chenye ubora, na amewaahidi mashabiki wake wake mkao wa kula anatarajia kutoa ngoma yake hivi karibuni.                      
Mwanamuziki wa kizazi kipya Chidi Benzi akiwaburudisha mashabiki wake na kuwa acha midomo wazi Kwa kazi nzuri alioifanya katika tamasha la muziki Mnene katika  klabu  ya New Msasani Jijini Dar es Salaam.
Mwanamuziki wa kizazi kipya  Izzo Business akifanya yake jukwaani    kuwaburudisha mashabiki  wake na wapenzi wa hip hop waliojitokeza Kwa wingi katika tamasha hilo la muziki mnene katika  klabu  ya New Msasani Jijini Dar es Salaam.
Mwanamuziki wa kizazi kipya Nuhu Mziwanda akizima kiki na kuwasha muziki katika kuhakikisha wakazi wa Kinondoniwanapata Burundi  kabambe akiimba  nyimbo yake mpya ambayo inajulikana kama  bao  la ushindi katika tamasha hilo la  muziki mnene katika  klabu  ya New Msasani Jijini Dar es Salaam.
Mwanamuziki wa kizazi kipya  kundi La Masada sita  wakitia burudani Kwa kuimba na kucheza kuwaburudisha wazi wa maeneo hayo  ambao hawakuachwa salama Kwa shoo nzuri iliofanywa na wadada hawa katika tamasha la  muziki mnene katika  klabu  ya New Msasani Jijini Dar es Salaam.

Mashabiki na wakazi wa Kinondoni waliojitokeza Kwa wingi kushuhudia shoo ya kukata na shoka kutoka Kwa wasanii Mbalimbali wa hapa nchini wakitoa burudani  kwao katika tamasha la  muziki mnene katika  klabu  ya New Msasani Jijini Dar es Salama. Picha na Na Agness Francis, Blogu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...