MUUNGANO wa Umoja wa Masoko ya Mkoa wa Dar es Salaam (MUMADA) wakiongozwa na Mwenyekiti wao Mohamed Mwekya wamekabidhi kilo za mchele 2835, Kilo 600 za Maharage pamoja Chumvi kwa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kwa lengo la kuunga mkono jitihada za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda katika ujenzi wa ofisi za walimu.


Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Mwenyekiti wa MUMADA, Mwekya amesema kuwa wao kama wafanyabishara wameguswa na harakati za RC Makonda katika kuboresha elimu hususani mazingira ya walimu, hivyo wameamua kutoa mchango wao huo ambao wana imani utasaidia.

Mwekya amesema wataendelea kushirikiana na na serikali katika shughuli mbalimbali za maendeleo na kuwataka wadau wengine wa maendeleo waunge mkono jitihada hizo zenye lengo ya kuboresha elimu kwa walimu kukaa ofisi zenye hadhi na taaluma yao.

Nae Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana, Mwajuma Magwiza amesema kuwa mchango huo utakwenda kwa shughuli iliyokusudiwa na wana imani kila mmoja akijitolea watatimiza lengo la kujenga ofisi 19 za walimu katika wilaya ya Kinondoni.
 Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana, Mwajuma Magwiza akipokea msaada vya vyakula kutoka kwa Mwenyekiti wa MUMADA, Mohamed Mwekya ikiwa kuunga mkono jitihada za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda katika ujenzi wa ofisi za walimu.

 Sehemu ya msaada vyakula kwa ajili ya watu wataofyatua tofali kwa ajili ya ujenzi ofisi za walimu.

.Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na Vijana, Mwajuma Magwiza akiwa katika ya pamoja na Muungano wa Umoja wa Masoko ya Mkoa wa Dar es Salaam (MUMADA) leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii)




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...