Mshindi wa kwanza katika mashindano ya  uandishi bora  wa habari za sayansi na kilimo (Biotchnolojia) katika kuendeleza Kilimo, Gerald Kitabu (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Elimu , Sayansi,Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce Ndalichako mara baada ya kumkabidhi cheki ya Dola 1500 kwa kuwa mshindi wa mashindano ya uandishi bora wa habari za Sayansi makabidhiano hayo yamefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Tume ya Sayansi (Costech) jijini Dar es Salaam leo.

Katika tuzo hizo Mshindi wa Kwanza amezawadiwa cheki ya Dola 1500, wapili dola 1200 na watatu Dola 100o na wengine Dola 750, 375 na 250 pia baadhi ya Vyombo vya habari wamezawadiwa cheti cha Shukrani kwa kuchapisha kazi za Sayansi na Kilimo.

Ukiacha Gerald Kitabu wengine ni Kelvin Gwabara, Innocent Mugune, Coletha Makurwa, Shadrack Sagati, Elias  Msuya, Fatma Abdul, Lucy Ngowi, Restuta Damian, Heren Kwavava, Daniel Sembelya na Zakaria Gabriel. 
Baadhi ya washindi wa Tuzo za uandishi mahiri wa habari za Sayansi  na Kilimo(Bioteknolojia) wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Elimu ,Sayansi,Teknolojia na Ufundi Prof.Joyce Ndalichako na  Mkurugenzi Mkuu wa Costech, Hassan Mshinda katika hafla ya kuwazawadia washindi wa habari waliofanya vizuri zaidi kwenye kuandika na kuelimisha umma kuhusu matumizi ya Sayansi, Teknologia na ubunifu hususani Bioteknologia katika kuendeleza kilimo.
Waziri wa Elimu , Sayansi,Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce Ndalichako akimkabidhi Kelvin Gwabara tuzo yake wakati aliposhinda tuzo ya uandishi bora wa habari za Sayansi na kilimo kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Costech, Hassan Mshinda katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Costech jijini Dar es salaam leo. Mkurugenzi Mkuu wa Costech, Hassan Mshinda

Waziri wa Elimu , Sayansi,Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce Ndalichako akimkabidhi hundi ya Dola 750 wakati aliposhinda tuzo ya uandishi bora wa habari za Sayansi na kilimo kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Costech, Hassan Mshinda katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Costech jijini Dar es salaam leo.
Waziri wa Elimu , Sayansi,Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce Ndalichako, Mkuu Mkuu wa Tume ya Sayansi na Technologia, (COSTECH)Hassan Mshinda na Mkurugenzi wa TBC wakiwa katika picha ya pamoja na Washindi wa tuzo za umahili bora wa habari za Sayansi na Kilimo jijini Dar es Salaam leo.
Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamaii
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...