Na Mathias Canal, Kilimanjaro

Wakulima wadogo katika Halmashauri ya Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro wameipongeza Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) yenye makao makuu yake nchini Nigeria kwa teknolojia walizoanzisha za kutafiti wadudu waharibifu na aina mpya ya mbegu za maharagwe aina ya Jesca, Lyamungo 90 na Uyole njano wanazozitoa kwa wakulima.

Wakulima hao wamesema kuwa mbegu hizo zimepelekea kuongezeka kwa uzalishaji wa mazao ya mbogamboga jamii ya mikunde huku katika Wilaya hiyo uzalishaji wa maharagwe ukiwa ndio ukombozi kwa wakulima kufuatia mafunzo na mbinu bora za kisasa wanazopatiwa na wataalamu wa (IITA) kupitia mradi wa N2AFRICA.

Wakizungumza kwa niaba ya wakulima wengine 30 katika Wilaya ya Hai Wanufaika wa mradi wa N2AFRICA Hashim Abdallah mkazi wa kitongoji cha Landi na Lucy David mkazi wa Kitongoji cha Madukani Kata ya weruweru wanasema kabla ya mradi huo walikuwa wanapanda kilo 60 za mbegu katika heka moja na mavuno ya gunia 3 mpaka 5 ambapo hivi sasa matarajio ya mavuno yao yataongezeka maradufu kwani wanatumia kilo 30 za mbegu kwenye heka moja na kuvuna gunia 10 mpaka 15.

Wakulima hao wameomba mafunzo ya kutengeneza mbegu bora za kilimo cha mbogamboga na mafunzo ya jinsi ya kuhifadhi mbegu hizo ili waweze kuendeleza uzalishaji wao wenyewe badala ya kuomba tena mbegu kutoka katika mradi huo wa N2AFRICA.

Lucy David akielezea jinsi alivyonufaika Mbegu za maharagwe zilizotolewa na Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) kupitia mradi wa N2AFRICA

Mkulima wa zao la maharagwe aliyenufaika na mbegu zilizotolewa na Mradi wa N2AFRICA Katika Kijiji cha Kikavu Chini, Kata ya Weruweru Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Hashim Abdallah akiwa shambani kuendelea na shughuli zake za kusafisha majani katika shamba lake kabla ya mavuno.

Wataalamu Kutoka Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) wakikagua shamba la Mkulima wa zao la maharagwe aliyenufaika na mbegu zilizotolewa na Mradi wa N2AFRICA Katika Kijiji cha Kikavu Chini, Kata ya Weruweru Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Hashim Abdallah.
Mkulima wa zao la maharagwe aliyenufaika na mbegu zilizotolewa na Mradi wa N2AFRICA Katika Kijiji cha Kikavu Chini, Kata ya Weruweru Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Mwantumu Abdillah akiwa shambani kuendelea na shughuli zake za kusafisha majani katika shamba kabla ya mavuno.
Mkulima wa zao la maharagwe Lucy David Katika Kitongoji cha Madukani, Kata ya Weruweru Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro akielezea mafanikio aliyoyapata kutokana na Mradi wa N2AFRICA, Wengine ni Wataalamu Kutoka Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) walipomtembelea shambani kwake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...