BAADA  ya kupata pointi 4 ugenini Yanga yarudi kwa kasi na kufanikiwa kunyakuwa pointi tatu ikiwa nyumbani kwa kuifunga Ndanda ya Mtwara goli 1-0.

Yanga wakiwa nyumbani waliweza kumiliki mpira kwa dakika zote 45 za kipindi cha kwanza na kufanikiwa kupata ushindi wa goli 1-0 lililofungwa na Ibrahim Ajib dakika ya 35.

Kutokana na matokeo ya leo Yanga wanakuwa sawa na Simba kwa pointi wakitofautiana kwa magoli ya kufunga.

Kwa upande wa kocha msaidizi wa Yanga, Shedrack Nsajigwa amesema watafanyia marekebisho mapungufu yaliyojitokeza licha ya kupata pointi 3.

Nae kocha msaidizi wa Ndanda Musa Mbaya amesema kushindwa kwao leo ni kutokana na ugeni wa wachezaji ambao wameingia kwenye kikosi chao na kupelekea kutoweka muunganiko mzuri hivyo makosa hayo  watayafanyia kazi mapungufu hususani kwenye upande wa ushambuliaji.
 Mshambuliani wa Timu ya Yanga, Ibrahim Ajibu, akiachia shuti kali kueleka langoni mwa timu ya Ndanda "Wanakuchele", katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara, iliyochezwa jioni ya leo kwenye dimba la Uhuru, Jijini Dar es salaam. Yanga imeshinda bao 1-0.
 Mabeki wa timu ya Ndanda, wakimdhibiti vilivyo, mshambuliani wa timu ya Yanga, Obrey Chirwa katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara, iliyochezwa jioni ya leo kwenye dimba la Uhuru, Jijini Dar es salaam. Yanga imeshinda bao 1-0.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...