Mkurugenzi wa taasisi ya Binti Foundation Johari Sadiq akizungumza mapema leo mbele ya Wanahabari (hawapo pichani),Katika hafla fupi ya utoaji wa msaada wa vifaa vya shule mbalimbali katika shule ya msingi ya Hananasisifu,jijini Dar,ikiwa ni sehemu yao ya kuadhimisha siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike,ambapo Kitaifa inaadhimishwa mkoani Mara,Pichani kulia ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo ya Hananasifu  Idda Uisso.
 Mkurugenzi wa taasisi ya Binti Foundation Johari Sadiq akimkabidhi Mwalimu Mkuu Idda Uisso baadhi ya vifaa vya shule ikiwemo Madaftari,Sale za Shule,Kalamu na vinginevyo kwa ajili ya wanafunzi ambao wanaishi katika mazingira magumu na hawajiwezi.Binti Foundation imetoa msaada huo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike,ambapo Kitaifa inaadhimishwa mkoani Mara.
 Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Hananasisifu Idda Uisso akitoa neno la shukurani kwa taasisi ya Binti Foundation kwa msaada wao walioutoa kwa shule hiyo,Mwalimu Idda ameziomba taasisi nyingine zenye uwezo kujitokeza kuwasadia watu mbalimbali wakiwemo wanafunzi wasiojiweza.
Mkurugenzi wa taasisi ya Binti Foundation Johari Sadiq na baadhi ya wadau wa taasisi hiyo wakishiriki kwa pamoja kugawa vifaa vya shule kwa wanafunzi mbalimbali ambao wanaishi katika mazingira magumu na hawana uwezo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Pongezi za kipekee ziwafikie Binti Foundation kwa moyo mzuri wa kuwasaidia watoto wa kike wanaoishi katika familia duni

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...