Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii .
MKUU wa Wilaya ya Same, Rosemary Sinyamule   amepokea Msaada wa  vifaa vyenye thamani ya Tshs. 10M  kutoka Benki ya NMB kwa  kwa ajili ya ujenzi wa Choo cha Wanafunzi wa Kike katika shule ya sekondari Kazita iliyopo kata ya Mhezi Same.

akizungumza wakati wa kupokea Msaada huo DC  Sinyamule  aliwashukuru NMB kwa vifaa hivyo vilivyojumuisha mabati, cement, mchanga, tofari, mawe, rangi na masink ya choo ambayo yatasaidia kwa kiasi kikubwa kumaliza tatioz la uhaba wa vyo vya watoto wa kike shuleni hapo. 

Dc Sinyamule aliwataka viongozi kuanzia bodi ya shule hadi Halmashauri kusimamia ujenzi wa vyoo hivyo na vikamilike kwa siku 45. Ili mwezi Novemba mwishoni tufanye uzinduzi wa vyoo hivyo. 

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya Aliwakumbusha fursa zilizopo Same kuwa ni pamoja na kufungua matawi mengine ya benki maeneo ya Ndungu na Mamba myamba kwani Wilaya inaendelea na uwekezaji mkubwa katika maeneo hayo. 

Naye meneja wa Benki hiyo Ndugu Mpimbi alieleza Benki hiyo ilivyoboresha huduma na kuwa ni benki inayoongoza kwa kurudisha faida kwa wateja katika mahadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja . 

alimaliza  kwa  kusema kuwa Kukamilika kwa vyoo hivyo kutafanya shule hiyo kutokuwa na upungufu tena wa vyoo jambo ambalo litasaidia sana watoto wa kike. 
Mkuu wa Wilaya ya Same, Rosemary Sinyamule akipokea  Vifaa vya ujenzi na Saruji kutoka kwa Meneja wa NMB Wilaya ya Same.
Sehemu ya Vifaa vya ujenzi vilivyotolewa na Benk ya NMB W ilaya ya Same
akiwa katika picha ya pamoja na Watendaji wa Benki ya NMB Wilaya ya Same.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...