Na Mashirika
ya Kimataifa.
KAMISHNA wa
Tume ya Uchaguzi nchini Kenya Roselyn Akombe ametangaza kujiuzulu, siku saba kabla ya Uchaguzi mpya wa urais uliopangwa kufanyika Oktoba 26, 2017
Akombe
ametoa tangazo hilo akiwa jijini New York nchini Marekani, na kusema kuwa
hawezi kuendelea kufanya kazi katika Tume hiyo, aliyoielezea kugawanyika.
Aidha,
amedokeza kuwa mazingira ya sasa ya kisiasa hayawezi kuruhusu kufanyika kwa
Uchaguzi utakaokuwa huru na haki.
“Siwezi
kuendelea kufanya kazi, katika mazingira kaa haya, kila dalili zinaonesha wazi
kuwa Uchaguzi hauwezi kuwa huru na haki,” alisema Akombe akiwa Marekani.
Bi Akombe
aliondoka nchini Kenya siku ya Jumanne,
kwenda Dubai kushuhudia uchapishwaji wa karatasi za kupigia kura lakini akaamua
kwenda nchini Marekani, ambako pia ni raia wa nchi hiyo.
Kujiuzulu
kwa Bi. Akombe, ni pigo kwa Tume hiyo ambayo ilikuwa inamtegemea kuzungumza kwa
niaba yake na kuitetea mara kwa mara.
"Tume
ijitokeze wazi, iwe na ujasiri na kusema kuwa Uchaguzi huu hauwezi kuwa huru na
haki katika mazingira haya," aliongeza Akombe.
Amesema pia
alikuwa anapata vitisho kuhusu maisha yake na huenda asirejee nchini Kenya
katika siku za hivi karibuni.
Suba
Churchil, kiongozi wa mashirika ya kiraia amesema hali hii inaendelea kuzua
wasiwasi kuhusu Uchaguzi huo uliopangwa kufanyika wiki ijayo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...