Mhashamu Baba Askofu Jimbo Katoliki Singida,Edward Mapunda akiongoza misa ya ibada ya maadhimisho ya Jubilee ya miaka 50 tangu kuzaliwa kwa Parokia ya Kupaa Bwana Manyoni iliyofanyika katika viwanja vya kanisa hilo mjini Manyoni.

Na Jumbe Ismailly, MANYONI.

MHASHAMU Baba Askofu Jimbo Katoliki Singida,Edward Mapunda amewataka waumini wa madhehebu hayo kuondokana na tabia ya kutegemea wafadhili wakati wa utekelezaji na ukamilishaji wa miradi mbali mbali ya maendeleo na kuwataka watambue kuwa bwana bure amekufa na aliyebakia kwa sasa ni bwana kujitegemea peke yake. Mhashamu Baba Askofu ametoa wito huo kwenye misa takatifu aliyoiongoza wakati wa maadhimisho ya sherehe za Jubilee ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Parokia ya Kupaa Bwana Manyoni iliyofanyika katika viwanja vya Kanisa la Parokia hiyo mjini Manyoni.

“Lakini ninachotaka kusisitiza jambo moja la kujitegemea,jambo moja la kujitegemea..enh tumesikia wazee wetu hapa walichanga hela,wazee wetu walichanga hela….wazeeeeee mlichanga hela sasa na sisi tunataka kuchanga hela ninyi mbona mlichanga tunataka kujenga Parokia.”alisisitiza baba Askofu Mapunda.
baadhi ya viongozi wa Parokia jimbo Katoliki Singida wakiwa katika maandamano ya kuadhimisha Jubilee ya miaka 50 tangu kuzaliwa kwa Parokia ya Kupaa Bwana Manyoni kwenye sherehe za maadhimisho hayo yaliyofanyika mjini,Manyoni.

Aidha Kiongozi huyo mkuu wa Kanisa hilo alisisitiza kwa wakazi wa wilaya ya Manyoni kwamba suala la kujitegemea halina budi kupatiwa kipaumbele katika shughuli za kukamilisha ujenzi wa majengo ya makanisa pamoja na vigango. Akifafanua zaidi Baba Askofu huyo aliweka bayana kuwa jukumu la kukamilisha ujenzi wa makanisa ni la waumini wenyewe na wenye moyo ambapo hata hivyo aliwatoa hofu waumini wa Manyoni kwa kuweka wazi msimamo wake kuwa anaamini kabisa waumini wa Manyoni ni waumini wenye moyo wa dhati wa kukamilisha majengo hayo.

Kutokana na moyo huo walionao wana Manyoni,Baba Askofu huyo alitumia wasaa wa maadhimisho hayo ya miaka 50 ya Jubilee kwa kuwataka waumini wa Jimbo hilo la Manyoni wajitoe bila kujibakiza,ili mipango na mikakati waliyojiwekea katika Jubilee hiyo iweze kufanikiwa zaidi.

“Namkumbuka sana Askofu Balina,askofu Balina alikuwa wa jimbo Katoliki la Shinyanga tunamuombea kwa Mungu ametangulia kwa Mungu lakini alikuwa anawaambia wasukuma wenzake maneno mazuri sana,na mimi nataka niwaambie hayo wana Manyoni kwa sababu mikakati hii ni mizito,mipango hii ni mizito,maazimio haya ni mazito tusipojitoa yote yatakwama”alisema huku akishangiliwa na waumini.


baadhi ya waumini wa kanisa hilo waliohudhuria kuadhimisha miaka 50 tangu kuzaliwa kwa Parokia ya Kupaa Bwana Manyoni,iliyofanyika mjini Manyoni.Picha zote Na Jumbe Ismailly.

Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa madhehebu ya Kikatoliki askofu Banila alikuwa akiwaambia wanashinyanga kwamba bwana bure amekufa na kwa kutokana na kauli hiyo naye Baba Askofu Mapunda alitumia pia kauli hiyo kwa kuwaasa waumini wa jimbo hilo kwamba bwana bure amekufa na bwana misaada yupo taabani na hivyo aliyebakia ni bwana kujitegemea.
Hata hivyo Askafu Mapunda aliwatahadharisha waumini wa jimbo hilo kwamba suala la kujitegemea lina umuhimu wake na kwa hali hiyo hawana ujanja wa kulikwepa jukumu hilo la kuondokana na utegemezi na kwenda kwenye tabia ya kujitegemea wenyewe kutokana na changamoto nyingi zinazowakabili Mapadrii zikiwemo changamoto za kutokuwa na vyombo vya usafiri.

Naye Paroko wa Parokia  ya Kupaa bwana Manyoni Jimbo Katoliki Singida,Padri Thomasi Wambura  alisema mwaka jana ulikuwa mwaka wa Jubilee ya 100  wa Mapadri Tanzania mwaka huu wao nao wanaadhimisha miaka 50 ya Jubilee ya Parokia yao na mwaka ujao wa 2018 wataadhimisha Jubilee ya miaka 150 tangu ukristo ulipoingia nchini Tanzania.

Kwa mujibu wa Padri Wambura waumini wote wana wajibu wa kuyatekeleza yale yote waliyoaswa na Baba Asskofu kama mchungaji wao mkuu lakini hakusita kusisitiza kwamba wajibu walionao ni kuyatekeleza yale waliyoyapata katika ukrito. Kwa upande wao baadhi ya waumini wa Kanisa hilo,Elizabeth Mkyalu  alishauri kwamba fedha zilizochangwa na waumini wa kanisa hilo hazina budi kuanza shughuli zilizokusudiwa za ujenzi wa majengo hayo huku akionya tabia ya kusubiri wafadhili kwamba kwa namna moja au nyingine hukwamisha miradi iliyoanzishwa pale wanapojitoa au kutochangia.

Naye Flora Lyimo kwa upande wake alisema kwamba njia pekee ya kujikwamua kiuchumi na kijamii na kuhakikisha maeendeleo endelevu yanapatikana ni kujiamini na kusimama wenyewe kwa miguu yao na siyo kusubiri kusaidiw a na watu wengine kwani endapo watasubiri misaada upo uwezekano wa malengo waliyojiwekea kutokamilika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...