Muigizaji wa Filamu nchini, Elizabeth Michael "Lulu" akiwa katika Mahakama kuu Dar es salaam akisubiri kuanza kusikilizwa kwa kesi inayomkabili ya mauaji ya bila kukusudia.
Lulu anakabilia na kesi ya kifo cha aliyekuwa muigizaji mwenzake wa filamu za Kibongo, Marehemu Steven Kanumba aliyefariki dunia Aprili 7, 2012 jijini Dar es salaam. Kulia ni Mama wa Muigizaji huyo.
UPDATES.
Elizabeth
Michael "Lulu" akiwa katika Mahakama kuu Dar es salaam akisubiri akitafakari jambo kabla ya kuanza
kusikilizwa kwa kesi inayomkabili ya mauaji ya bila kukusudia
Muigizaji wa Filamu nchini, Elizabeth Michael "Lulu" akiwa katika Mahakama kuu Dar es salaam akisubiri kuanza kusikilizwa kwa kesi inayomkabili ya mauaji ya bila kukusudia. Lulu anakabiliwa na kesi ya kifo cha aliyekuwa muigizaji mwenzake wa filamu za Kibongo, Marehemu Steven Kanumba aliyefariki dunia Aprili 7, 2012 jijini Dar es salaam. Kulia ni Mama wa Muigizaji huyo.
Muigizaji wa Filamu nchini, Elizabeth Michael "Lulu" akiwa katika Mahakama kuu Dar es salaam akisubiri kuanza kusikilizwa kwa kesi inayomkabili ya mauaji ya bila kukusudia. Lulu anakabiliwa na kesi ya kifo cha aliyekuwa muigizaji mwenzake wa filamu za Kibongo, Marehemu Steven Kanumba aliyefariki dunia Aprili 7, 2012 jijini Dar es salaam. Kulia ni Mama wa Muigizaji huyo.
Na Karama Kenyunko,Gblobu ya Jamii.
Shahidi
wa Kwanza wa upande Jamhuri katika kesi ya mauaji ya bila
kukusudia dhidi ya marehemu Steven Kanumba, inayomkabili msanii maarufu
nchini, Elizabeth Michael ameieleza mahakama kuu kuwa licha ya kumwambia
Lulu abaki na Kanumba yeye alipomfuata daktari lakini aliondoka na
kumuacha peke yake
Shahidi
huyo, Bosco Seth (30) ambaye pia ni mdogo wa Marehemu Kanumba ameyasema
hayo leo mapema mbele ya Jaji Sam Rumanyika wakati akitoa ushahidi wake.
Kabla ya kuanza kutolewa kwa ushahidi, Lulu alikumbushiwa mashtaka yake
ambapo ilidaiwa Aprili 7, mwaka 2012 huko Sinza Vatcan wilaya ya Kinondobi
alimuua bila kukusidia Kanumba, Lulu alikana shtaka hilo.
Akiongozwa
na Wakili wa serikali Faraja George, Bosco amesema baada ya
kupata taarifa za kudondoka kwa Kanumba kutoka kwa Lulu alimpigia simu
daktari wao aliyemtaja kwa jina la Paplas ambaye alimtaka kwenda
kumchukua Hospitalini kwake na kwa kuwa hakukuwa na usafiri aliwasha
Gari na kimfuata na kumuomba Lulu abaki na Kanumba.
Wakati
narudi na Dk, Lulu alinipigia simu akasema Kanumba nimemuwekea mpaka
maji kifuani lakini haamki ninaindoka, nikamwambia nisubiri lakini mpaka
nafika pale sikumkuta.
Alidai
baada ya Dkt kufika na kumpima alimshauri wampeleke Muhimbili, ambapo
kwa msaada wa jirani yao aliyemtaja kwa jina la Baraka walimbeba Kanumba
na kumuingiza kwenye gari hadi Muhimbili.
Amedai
wakati wanaangaika kumuingiza Kanumba kwenye gari, mama mwenye nyumba
alisikia akafungua mlango aliposikia tatizo nae aliwasha gari lake na
kutusindikiza, ambapo walienda moja kwa moja Emergency na baada
kumfanyia Kanumba uchunguzi Dr aliwaambia kuwa ameishafariki na
kutuambia tufuate taratibu za polisi.
Amedai
walienda polisi Urafiki ambako wakiwa huko Lulu alikuwa akimpigia Dkt Paplas Simu ndipo polisi wakamuomb Dkt aweze kuwasaidia kumpata Lulu
ambapo asubuhi ya Aprili 7, baada ya wao kumaliza kuhojiwa Lulu
alikamatwa.
Akielezea
jinsi tukio lilivyotokea alidai, Aprili 4 mwaka 2012 alishinda
nyumbani na kaka Kanumba toka asubuhi na ilipofika mida ya saa kumi
jioni, Kanumba alimuomba asitoke na wangetoka pamoja usiku wa saa sita.
Akadai
ilipofika saa sita kasoro za usiku, Kanumba alimwambia wajiandae watoke,
ambapo yeye alikuwa wa Kwanza kumaliza kujiandaa lakini alipotoka
chumbani kwake akielekea sebuleni, alikutana na Kanumba akipita kwenye
koridoni huku akiwa amevalia taulo kuelekea sebuleni, akipaka Mafuta
kichwabi, sebuleni kwa nje kulikuwa na Gari la Lulu, nikamuuliza mbona
tunachelewa akanijibu sasa hivi tunaondoka.
Akadai
kuwa, Kanumba ndiye alimfungulia mlango lulu, waliingia wote ndani
akiwa chumbani kwake ambako alirudi kumsubiria Kanumba huku mlango wake
ukiwa wazi kidogo, wakati wakitembea Koridoni kuelekea chumbani kwa
Kanumba alisikia wakigombana huku Kanumba akimuuliza lulu kwa nini
anaongea na boyfriend wake mbele yake.
Aliendelea
kudai kuwa muda wote huo walikuwa wakivutana, Lulu akitaka kutoka nje
na Kanumba akimvutia ndani mara waliingia chumbani na mlango ukafungwa.
Nilisikia sauti za kupigana na muda mfupi kidogo Lulu alifungua mlango
na kuja chumbani kwangu akasema, Kanumba amedondoka sijui amekuwaje
Alidai
aliondoka hadi chumbani kwake, alimkuta Kanumba amedondoka kwa kuegemea
ukuta huku akiwa hawezi kupumua, (amesafocate), alimchukua na kumlaza
chini kisha akampigia simu Dkt Paplas, kulikuwa na alama mbili za nywele
zilizokuwa zinaonyesha kuwa alipoburuzika,
Alidai, Mazingira ya chumba hicho cha kaka yake yalikuwa ya kawaida kama Siku zote.
alidai baada ya hapo aliwasha gari na kwenda kumchukua Dkt ndipo Lulu akanipigia simu na kusema Kanumba haamki. Kisha
Wakili wa utetezi, Peter Kibatala alimuuliza Shahidi kama ushahidi
aliotoa mahakamani unafanana na maelezo ya polisi alisema
ndio, Kibatala
alimuuliza shahidi huyo ni wapi aliwaeleza polisi kuwa alimuacha
mshtakiwa Lulu peke yake na Marehemu Kanumba wakati anaenda kumtafuta Dkt. Paplas alisema hakuwaeleza.
Akaongeza kuwa yeye alikuwepo kwenye postmotam ya kawaida na wala hakuwepo wakati wakichukua sampuli za mwili kupeleka maabara.
Kesi itaendelea kesho Oktoba 20, 2017.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...