Na Veronica Simba - Dodoma

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu, amelitaka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuhakikisha linawajibika ipasavyo kwa wateja wake ili kukuza imani yao kwa shirika hilo.

Akizungumza na viongozi mbalimbali wa shirika hilo wa Mkoa wa Dodoma, leo Oktoba 17, 2017, Naibu Waziri amebainisha kuwa mojawapo ya njia muhimu ya uwajibikaji kwa jamii ni kupitia utoaji taarifa kwa wateja kuhusu masuala mbalimbali yanayowahusu.

“Mathalani, kunapokuwa na katizo la umeme, wateja walioko eneo husika wanapaswa kutaarifiwa kabla ya katizo hilo ili wajipange,” alisisitiza.

Ameeleza njia nyingine ya shirika hilo kuwajibika kwa jamii, kuwa ni kushughulikia matatizo mbalimbali ya wateja wao kwa wakati na kuachana na utaratibu wa kufanya kazi kwa mazoea.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akizungumza na wafanyakazi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Dodoma (hawapo pichani), alipowatembelea kwa lengo la kujitambulisha kwao na kueleza vipaumbele vyake vya kazi.
Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Dodoma, Zakayo Temu (kushoto), akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi wa Ofisi yake kwa Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (kulia), wakati Naibu Waziri alipotembelea Ofisi hiyo na kuzungumza na viongozi.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (aliyesimama) akizungumza na viongozi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Dodoma, alipotembelea Ofisi hizo leo Oktoba 17, 2017.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...