Waziri wa kazi, ajira, sera, bunge, vijana na wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amelipongeza Shirika la NSSF kwa kuwa mfano wa kuigwa katika nyanja za kiuchumi na kijamii. Waziri mkuu aliyasema hayo katika mkutano wa wadau wa NSSF unaoendelea katika Kituo cha kimataifa cha mikutano AICC, Arusha

Waziri wa kazi pia alipongeza NSSF kwa kuandaa mkutano wa wadau unaofanyika hapa jijini Arusha, alisema mkutano huo siyo muhimu kwa NSSF na wadau tu bali pia kwa maendeleo na ustawi wa Taifa letu. Pia alifurahi kupata  nafasi ya kufuatilia utendaji wa NSSF pamoja na kuona moja kwa moja kutoka kwa wadau wa NSSF.
Pia aliwapongeza  wadau wa NSSF kwa kuitikia wito wake wa kuja kushiriki ili kupata taarifa za utekelezaji wa maazimio waliyokubaliana mwaka jana, taarifa za utendaji na kuchangia mawazo yatakayoleta tija ya kulijenga Shirika. Aidha, aliwapongeza Wageni mbalimbali katika mkutano huo ambao ni pamoja na Mhe. Anthony Mavunde, Katibu Mkuu Ndg. Eric Shitindi, Mkurugenzi Mkuu wa SSRA na Wakurugenzi wa Mifuko mingine ya Pensheni.

Vile vile Waziri wa kazi alitoa pongezi kubwa kwa namna ambavyo NSSF  ilivyojitolea katika kutekeleza jukumu la kukuza Uchumi wa Viwanda  kwani alisema Ujenzi wa Taifa si jukumu la Serikali Kuu peke yake bali ni la kila Mtanzania mmoja mmoja, taasisi na makampuni, na ndio maana NSSF pamoja na kuwa na jukumu la hifadhi ya jamii kwa mujibu ya sheria yake husika, imeona haja ya kupanua wigo wa uwekezaji wake na kuelekea katika viwanda jambo ambalo litaongeza ajira, kuongeza uzalishaji, na kukuza uchumi wa nchi kwa ujumla. 
 Waziri Mhagama alitoa  mfano katika uwekezaji wa NSSF  katika kukuza viwanda tumeshuhudia uwezekano wa kuzalisha ajira za moja kwa moja kwa Watanzania kutoka na uwekezaji ilioufanya katika viwanda mbali mbali. Nichukue fursa hii kuipongeza NSSF kwa kutoa mkopo wa shilingi bilioni 3.1 kwa lengo la kuongeza uzalishaji katika kiwanda cha madawa kilichopo Kibaha chini ya Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC). Katika kiwanda hiki ambapo ajira 100 zimezalishwa. Uzalishaji wa viuadudu ulianza Mwezi Desemba 2016 na mpaka sasa kiwanda kimezalisha jumla ya lita 327,400 ambazo ziliuzwa katika masoko ya ndani na nje.

Shirika lilitoa Mkopo kwa ajili ya upanuzi wa Kiwanda cha Chaki kilicho chini ya Usimamizi wa Halmashauri ya Maswa, Mkoani Simiyu mnamo mwezi June, 2017. Mkopo huu kwa ujumla utaongeza uzalishaji wa chaki kutokea vipande 432,000 vya chaki nyeupe (sawa na  Katoni 180) kwa siku hadi vipande milioni 4.8 vya chaki nyeupe na za rangi (sawa na Katoni 2,000) kwa siku. Ongezeko la uzalishaji huu wa chaki utasaidia kuendeleza Sera ya Serikali ya “Elimu Bila Malipo” kwani itasaidia kupunguza mahitaji makubwa ya chaki katika shule za awali na msingi. Jumla ya Ajira 100 za moja kwa moja zinatarajiwa kutokana na uwekezaji huu.
 Pia aliwapongeza NSSF kwa kushirikiana na PPF, na Jeshi la Magereza kupitia Kampuni ya Mkulazi, wamewekeza katika Mradi mkubwa wa shamba la miwa na Kiwanda cha Sukari kilichopo Mbigiri ambapo tayari hatua za upandaji miwa zimeanza nami nikiwa miongoni mwa j waliopata fursa ya kupanda miwa yamwanzo kabisa. 

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...